Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Kim Jong-un atishia kufuta mkutano wake na Trump

Korea Kaskazini imesema huenda ikaufuta mkutano kati ya kiongozi wake Kim Jong-un na Rais wa Marekani Donald Trump iwapo Marekani itaendelea kusisitiza kwamba taifa hilo la bara Asia ni lazima liharibu au kusalimisha silaha zake za nyuklia. Mkutano huo ambao umesubiriwa kwa hamu kati ya Bw Trump na Bw Kim unatarajiwa kufanyika mnamo 12 Juni. Hayo yamejiri baada ya Korea Kaskazini kusema imejitolea kuhakikisha silaha za nyuklia zinaondolewa katika rasi ya Korea. Maandalizi ya mkutano huo wa Trump-Kim yamekuwa yakiendeleza, lakini sasa kumeingia shaka kuhusu hilo. Shirika la habari la serikali ya Korea Kaskazini KCNA limemnukuu naibu waziri wa mambo ya nje Kim Kye-gwan akisema iwapo Marekani "itatubana na kusisitiza kwamba ni lazima tusalimishe bila masharti silaha zetu za nyuklia basi hatutakuwa tena na hamu ya kushiriki mazungumzo hayo na itatulazimu kutafakari upya iwapo tutakubali mkutano unaotarajiwa kufanyika karibuni kati ya DPRK-US. Korea Kaskazini kir...

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 15.05.2018

Jonjo Shelvey Kiungo wa kati wa Newcastle Jonjo Shelvey, 26, hatajumuishwa kwenye kikosi cha Uingereza kitakachoshiriki kombe la dunia kutokana rekodi yake mbaya kinidhamu. (Mirror) Manchester United wako tayari kuilipa Napoli pauni milioni 44 kumpata beki Elseid Hysaj msimu huu. Raia huyo wa Albania wa umri wa miaka 24 atakuwa mlinzi namba saba ghalia zaidi duniani. (Sun) Everton watamfuta meneja Sam Allardyce saa 48 zinazokuja na wanakaraibia kumteua aliyekuwa meneja wa Watford Marco Silva. (Mirror) Sam Allardyce Afisa mkuu mtendaji wa Arsenal Ivan Gazidis na mkrugeni mkuu Josh Kroenke wamemtambua kiungo wa kati wa zamani wa Arsenal Mikel Arteta ambaye sasa ni kocha huko Manchester City kama mtu anayeweza kuchukua mahala pake Arsene Wenger kama meneja wa Arsenal. (Mail) Meneja wa Juventus Massimiliano Allegri bado anaweza kuwa meneja wa Arsenal ikiwa atashinda vita vya kuhama wachezaji. (Star) Arsenal: Pierre-Emerick Aubameyang Mshambulizi wa Arsena...

Utafiti: Wanawake wa Rwanda na Kenya ndio wataishi muda mrefu zaidi Afrika Mashariki

Wanawake nchini Rwanda na Kenya ndio wanaotarajiwa kuishi muda mrefu zaidi miongoni mwa wanawake na wanaume katika nchi za Afrika Mashariki, kwa mujibu wa takwimu. Umri wa wanawake kuishi Rwanda kwa sasa ni miaka 69.3 na nchini Kenya ni miaka 69.0. Hata hivyo, umri wa kuishi wa wanaume Uganda ndio ulioongezeka zaidi katika kipindi cha mwongo mmoja uliopita, ambapo umepanda kwa miaka 13.5. Nchini Tanzania, umri wa kawaida wa kuishi kwa wanawake kufikia mwaka 2016 ulikuwa miaka 66, ongezeko la miaka 10 ukilinganisha na mwaka 1990 kwa mujibu wa Utafiti wa Mzigo wa Maradhi Duniani mwaka 2016, ulioratibiwa na Taasisi ya Takwimu za Afya na Utathmini. Kwa wanaume, umri wa kuishi ulikuwa miaka 62.6 kufikia mwaka 2016 ukilinganisha na miaka 53.7 mwaka 1990. Kwa kiwango cha kadiri, umri wa kuishi kwa Watanzania umeongezeka kwa miaka kumi kufikia sasa tangu mwaka 1990. Nchini Kenya, umri wa kuishi kwa wanawake umeongezeka kutoka miaka 62.6 mwaka 1990 hadi miaka 69 mwaka 2016,...

Zarif afanya juhudi za kuokoa makubaliano ya kinyuklia

Waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Javad Zarif amesema nchi yake itahitaji uhakikisho kutoka mataifa mengine yenye nguvu  duniani iwapo iendelee kutekeleza mkataba wa kinyuklia wa mwaka  2015, baada ya Marekani  ikujitoa. Waziri wa mambo  ya  kigeni  wa Urusi  Sergei Lavrov  alikutana  na  mwenzake huyo wa  Iran mjini Moscow  Jumatatu  kujadili kile  kinachoweza  kufanyika  kulinda makubaliano  hayo  na  Iran  baada  ya  uamuzi  wa  rais  wa Marekani Donald Trump kujitoa  katika  mkataba  huo.  Waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Mohammad Javad Zarif Iran  jana  iliupa  Umoja  wa  Ulaya  siku  60 kutoa uhakikisho wa kuendelea  na  utekelezaji  wa  makubaliano  hayo  ya  kinyuklia baada...

Hali tete ya kiusalama eneo la Turkana Kenya

Majambazi waliokuwa na silaha wamewaua maafisa wawili wa polisi wa akiba huko Kapedo, Turkana Mashariki Mkasa mwingine umelikumba bonde la Ufa nchini Kenya baada ya majambazi waliojiami kuwaua maafisa wawili wa polisi wa akiba huko Kapedo, Turkana Mashariki. Mkasa huu unakuja siku nne baada ya mauaji ya watu wanne, watatu wakiwa wanafunzi walioshambuliwa wakielekea shuleni katika eneo hilo. Viongozi wa kisiasa sasa wanatupiana lawana za uchochezi huku ikielezwa kuwa huenda mgogoro wa eneo hilo umebadilika kutoka wizi wa mifugo na kuhamia kwenye ugonvi wa mipaka. Mauaji ya maafisa 21 wa polisi katika eneo la Kapedo mwezi Oktoba mwaka 2014 uliliweka eneo hili katika ramani ya ukosefu wa usalama, hali iliyofanya mahusiano kati ya jamii mbili zilizoko eneo hilo kuwa mbaya zaidi, kila jamii ikijivua lawama. Mwaka uliopita serikali kupitia wizara ya usalama wa ndani ilitekeleza oparesheni katika eneo hilo kukabiliana na mauaji na mashambulizi, lakini wakaazi wanasema bado usalama hau...

Uingereza yatakiwa kuweka bayana msimamo wake juu ya Brexit

Umoja wa Ulaya umeionya Uingereza kuwa muda unayoyoma wa kufikia makubaliano juu ya mpango wa kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya maarufu kama Brexit. Umoja wa Ulaya umesema Uingereza inapaswa kuhakikisha kuwa haijiondoi kwenye Umoja huo mwezi Machi mwaka ujao bila ya makubaliano, hatua inayoongeza shinikizo kwa Waziri Mkuu Theresa May. Lakini kwa upande wake msemaji wa May,  amesema kinachopewa kipaumbele kwa sasa ni kutekeleza jambo hilo kwa makini na sio kukimbizana na muda. Wanadiplomasia na maafisa mjini Brussels wamesema kumekuwepo na maendeleo kidogo katika majadiliano ya Brexit tangu siku ya mwisho ya mkutano wa viongozi wa Umoja wa Ulaya, na kuanza kutilia mashaka iwapo Umoja huo na Uingereza wataweza kufikia hatua nyengine muhimu katika mkutano wao wa kilele utakaofanyika June 28 na 29. Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May "Tuna wasiwasi kwamba hakuna msimamo wa wazi kutoka kwa Uingereza, muda unayoyoma, tunahitaji kupiga hatua muhimu lakini hilo halijafanyika, ki...

Israel yasema ubalozi mpya mjini Jerusalem ni Historia

Marekani imeufungua rasmi ubalozi wake mpya katika mji wa Jerusalem huku Wapalestina zaidi ya 40 wakiuwawa na mamia wengine wakijeruhiwa kwenye mapambano na askari wa Israel katika harakati za kuipinga hatua hiyo. Hatua ya Marekani ya kuuhamishia rasmi ubalozi wake kwenye mji  wa Jerusalem kutoka Tel Aviv imetekelezwa baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kuitambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel. Balozi wa Marekani nchini Israel David Friedman amesema kuwa baada ya miaka 70 ya kuanzishwa kwa taifa la Israel wakati muhimu kama huu na wa kihistoria ni kwa sababu ya ujasiri wa mtu mmoja tu ambaye ni rais wa Marekani Donald Trump. Rais huyo wa Marekani hakuhudhuria sherehe hizo lakini alitoa hotuba kupitia kwenye Video. Trump amesema Marekani itaendelea kujitolea kikamilifu katika kuuwezesha mpango wa amani wa Mashariki ya Kati. Jared Kushner mkwe wa Trump na mke wake Ivanka binti yake Tru...