Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Zarif afanya juhudi za kuokoa makubaliano ya kinyuklia

Waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Javad Zarif amesema nchi yake itahitaji uhakikisho kutoka mataifa mengine yenye nguvu  duniani iwapo iendelee kutekeleza mkataba wa kinyuklia wa mwaka  2015, baada ya Marekani  ikujitoa.



Waziri wa mambo  ya  kigeni  wa Urusi  Sergei Lavrov  alikutana  na  mwenzake huyo wa  Iran mjini Moscow  Jumatatu  kujadili kile  kinachoweza  kufanyika  kulinda makubaliano  hayo  na  Iran  baada  ya  uamuzi  wa  rais  wa Marekani Donald Trump kujitoa  katika  mkataba  huo. 


Waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Mohammad Javad Zarif

Iran  jana  iliupa  Umoja  wa  Ulaya  siku  60 kutoa uhakikisho wa kuendelea  na  utekelezaji  wa  makubaliano  hayo  ya  kinyuklia baada  ya  uamuzi  huo  wa  Marekani kujitoa. "Lengo  lililokusudiwa la  mazungumzo  ni kupata  uhakikisho kwamba  maslahi  ya  watu  wa Iran, yatalindwa," Zarif  alisema  katika  mkutano  na  mwenzake  wa Urusi, Sergei  Lavrov, kwa  mujibu  wa  shirika  la  habari  la  Urusi TASS.

Lavrov alisisitiza  kwamba  Urusi  na  wadau  wengine  katika mkataba  huo  wa  kinyuklia  wanania  ya  kuuendeleza, ujumbe ambao  umerejewa  pia  katika  matamshi  kutoka  Umoja  wa  Ulaya yaliyotolewa  na  waziri  wa  masuala   ya  Ulaya  wa  Ujerumani Michael Roth.

"Shirikisho  la  Urusi  pamoja  na  washiriki  wengine  katika  mkataba huo  wa  kinyuklia, China, mataifa  ya  Ulaya, pia  wana maslahi halali  ambayo  yamo  katika  makubaliano  hayo  yaliyoidhinishwa  na baraza  la  Usalama  la  Umoja  wa  Mataifa, " alisema  Lavrov.

"Leo tunamatumaini  kuona ushiriki  wa  mataifa  ya  Ulaya, China, Urusi, Iran  na  Umoja  wa Ulaya  kwa  kutumia  utaratibu  uliopo kutoruhusu  kuporomoka  kwa  waraka  huu  muhimu, kutoruhusu kuivuruga  hali  katika  eneo  la  mashariki  ya  kati, kutoruhusu vitisho  vipya  katika udhibiti  wa  kusambaa  kwa  silaha  za kinyuklia."

Waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza Boris Johnson akimpokea waziri mwenzake wa Iran Javad Zarif (Kulia)

Russia  ambayo  ina  uhusiano  imara  na  Iran, ilikuwa  mpatanishi katika  kupatikana  kwa  makubaliano  hayo  ya  mwaka  2015 yenye lengo  la  kuizuwia  Iran  kujipatia  silaha  za  kinyuklia.

Katika  mkutano  mjini  Beijing  mwishoni  mwa  juma, waziri  wa mambo  ya  kigeni  wa  China Wang Yi alimuahidi Zarif kwamba China  itaendelea  kufanyakazi  kuendelea  na  makubaliano  hayo.

Waziri wa mambo  ya  kigeni  wa  Iran Mohammed Javad Zarif amesema  mpango  wa  pamoja  wa  kuchukua  hatua , uliotiwa  saini mwaka  2015 ulikuwa  katika  msingi  wa  uwiano  wa  majukumu  kati ya  upande  wa  Iran  na    kulinda  maslahi  ya  watu  wa  Iran  ikiwa  ni  pamoja  na  Marekani."

Waziri anayehusika na masuala ya Ulaya wa Ujerumani Michael Roth

Mpango wa pamoja  wa  kuchukua  hatua uko  katika  msingi  wa uwiano wa  majukumu  kati  ya  upande wa  Iran na  Ulaya  ikiwa  ni pamoja  na  Marekani. Baada  ya  Marekani  kujitoa  uwiano  huu uko  hatarini. Tunapaswa  kuona  vipi  tunaweza tunaweza kuulinda.

Mataifa  matatu ya  Ulaya, Ujerumani, Ufaransa  na  Uingereza yameomba  muda  wa  siku  90, duru mjini  Tehran zimesema. Suala hilo  linatarajiwa  kuzungumzwa  katika  mkutano  kati  ya  Zarif  na wenzake  wa  Umoja  wa  Ulaya  mjini  Brussels  kesho  Jumanne.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.