Rais Magufuli kuikabidhi Simba kombe la ubingwa wa VPL

mteulethebest







Rais wa Tanzani, John Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara (VPL) kati ya mabingwa wapya Simba SC na Kagera Sugar utakaochezwa Jumamosi Mei 19, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema wamemuandikia barua Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kumuomba Rais Magufuli awe mgeni Rasmi kwenye mchezo huo.

Karia ameeleza kuwa Rais Magufuli endapo atakubali wito huo, atapata nafasi ya kuwakabidhi Simba Kombe la VPL, sanjari na kuikabidhi  Timu ya Taifa ya soka ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys  kombe la CECAFA kwa vijana walilotwaa siku za karibuni nchini Burundi.

Amesema mchezo kati ya Simba na Kagera Sugar utaanza saa 8:00 mchana badala ya Jumapili saa 10:00 jioni ili kutoa fursa kwa sherehe hizo kufanyika kikamilifu.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU