Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Visa vya Ebola vyaongezeka Congo


Wizara ya afya ya nchini Congo imesema idadi ya visa vya homa ya Ebola vilivyothibitishwa nchini humo vimeongezeka kutoka watu watatu na kufikia watu 14.


Wizara hiyo imesema mtu mmoja pekee ndiye aliyethibitishwa kufariki dunia ingawa kuna madai kwamba watu 25 wamefariki.


Maafisa wa afya wako mbioni kuidhibiti homa hiyo inayosambazwa na virusi na ambayo kwa sasa imethibitishwa katika mji wa Mbandaka wenye watu zaidi ya milioni moja. Mbandaka ni mji ambao hauko mbali na Mji Mkuu Kinshasa na uko katika Mto Congo ambao ni eneo lenye shughuli nyingi za usafiri.


Shirika la Afya Duniani, WHO limefanya kikao cha dharura leo na kutangaza kwamba tahadhari ya kuenea kwa maradhi hayo imeongezeka kutoka "juu" na sasa imefikia kuwa "juu mno". Shirika hilo linasema kuwa tahadhari katika nchi zilizoko katika kanda hiyo imeongezeka pia kutoka kiwango cha "wastani" na sasa imefikia kiwango cha "juu", ingawa tahadhari ya maradhi hayo kuenea dunia nzima inasalia kuwa ya "chini".


Visa 44 vya homa ya kuvuja damu vimerekodiwa


Kuzuka kwa Ebola kunasababisha kujaribiwa kwa chanjo mpya ya Ebola ambayo ilionekana kufanya kazi vyema Afrika Magharibi miaka michache iliyopita. Zaidi ya vipimo 4,000 vya chanjo hiyo vimewasili nchini Congo wiki hii huku vipimo zaidi vikitarajiwa kufika. Changamoto kuu itakuwa kuiweka chanjo hiyo katika hali ya baridi katika eneo ambalo lina miundo mbinu duni na umeme katika sehemu chache.


Chanjo ya Ebola ikiingia nchini Congo


Julien Raickman ni Mkuu wa Madaktari wasio na Mipaka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.


"Tulijua jana kwamba kumethibitishwa kisa kimoja baada ya uchunguzi wa maabara katika mji wa Mbandaka. Kuanzia mwanzo wa kuzuka kwa maradhi haya," alisema Raickman. "Tumerekodi visa 44 vya homa ya kuvuja damu. Na ni homa ambayo tuliiona, visa vyote vitatu vya Ebola ambavyo vimethibitishwa," aliongeza Mkuu huyo wa MSF.


WHO itaita kikao cha wataalam wa kamati ya dharura baadae leo


Jambo ambalo linadhibitiwa lisitokee kwa sasa ni kuzuka kwa Ebola katika mji wa Kinshasa, mji wenye mamilioni ya watu ambao wengi wao wanaishi katika nyumba za mabanda zisizo na mfumo wa kutoa maji machafu.


Watu wengi Congo wanaishi katika mitaa ya mabanda isiyo na hali bora ya usafi


Baadae leo, WHO itaita kikao cha wataalam wa Kamati ya Dharura kutoa ushauri kuhusu njia za kimataifa za kulikabili janga hilo na iamue iwapo itabuni mpango wa dharura wa kushughulikia wasiwasi wa kimataifa kuhusiana na Ebola.


Tangu mwaka 1976, huu ni mlipuko wa tisa wa Ebola nchini Congo. Virusi vya ugonjwa huu vinasambazwa kwa watu kutoka kwa wanyama wa porini wakiwemo popo na tumbili. Hakuna tiba maalum ya Ebola. Dalili zake ni homa, kutapika, kuharisha, maumivu ya misuli na wakati mwengine kuvuja damu ndani na nje ya mwili. Ebola inaweza kusababisha vifo katika asilimia 90 ya visa


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...