Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Israel yasema ubalozi mpya mjini Jerusalem ni Historia

Marekani imeufungua rasmi ubalozi wake mpya katika mji wa Jerusalem huku Wapalestina zaidi ya 40 wakiuwawa na mamia wengine wakijeruhiwa kwenye mapambano na askari wa Israel katika harakati za kuipinga hatua hiyo.


Hatua ya Marekani ya kuuhamishia rasmi ubalozi wake kwenye mji  wa Jerusalem kutoka Tel Aviv imetekelezwa baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kuitambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.


Balozi wa Marekani nchini Israel David Friedman amesema kuwa baada ya miaka 70 ya kuanzishwa kwa taifa la Israel wakati muhimu kama huu na wa kihistoria ni kwa sababu ya ujasiri wa mtu mmoja tu ambaye ni rais wa Marekani Donald Trump. Rais huyo wa Marekani hakuhudhuria sherehe hizo lakini alitoa hotuba kupitia kwenye Video.

Trump amesema Marekani itaendelea kujitolea kikamilifu katika kuuwezesha mpango wa amani wa Mashariki ya Kati. Jared Kushner mkwe wa Trump na mke wake Ivanka binti yake Trump ambao ni wasaidizi wa rais huyo, waliuongoza ujumbe wa Marekani kwenye sherehe hizo.

Balozi wa Marekani nchini Israel David Friedman

Wakati sherehe hizo zilipokuwa zikifanyika Wapalestina waliendelea kufanya maandamano makubwa kwenye mpaka wa Gaza na Israeli. Kwa furaha kubwa tele waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amemsifu rais Trump na kumshukuru kwa kuileta historia hii.

Hatua ya kuhamishwa ubalozi wa Marekani nchini Israel kutoka mjini Tel Aviv na kuupeleka katika mji wa Jerusalem imewachukiza mno Wapalestina, ambao wanataka mji wa Jerusalem mashariki kuwa mji mkuu wa taifa la baadae la Palestina. Wizara ya Afya katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa zaidi ya Wapalestina 40 wameuawa huku wengine zaidi ya 1900 wakiwa wamejeruhiwa.

Ubalozi huo wa Marekani umefunguliwa mjini Jerusalem wakati amabpo Wapalestina wanaomboleza siku ya maafa ya Al-Naqba yaani siku ya kuundwa kwa taifa la Israel miaka 70 iliyopita tarehe 15 Mei.

Wakati huo huo serikali ya Ujerumani imeelezea wasi wasi wake juu ya mgogoro wa Mashariki ya Kati. Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani amesema kufunguliwa kwa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem kusiwe sababu ya kufanya ghasia. Msemaji huyo pia ameeleza kuwa Israel nayo inapaswa kuzingatia kanuni ya kujizuia. Katika tamko hilo Ujerumani imesema ina uhakika kwamba suluhisho juu ya suala la Jerusalem linaweza kupatikana kwa njia ya mazungumzo.

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Heiko Maas

Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Federica Mogherini ametoa mwito kuzitaka pande zote zijizuie na amesisitiza juu ya umuhimu wa suluhisho la nchi mbili baina ya Israel na Palestina.

Ufaransa pia imetoa mwito kwa pande zote kujizuia ili kupunguza maafa. Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa amesema haungi mkono hatua ya Marekani. Waziri mkuu wa Palestina Rami Hamdallah amesema uamuzi wa Marekani wa kuitambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel unakiuka sheria za kimataifa.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres naye ameelezea wasi wasi wake juu ya idadi ya watu waliouawa karibu na mpaka baina ya Ukanda wa Gaza na Israel. Wakati huo huo Umoja wa nchi za Kiarabu unatarajiwa kuitisha kikao cha dharura ili kujadili uamuzi wa Marekani. Naibu katibu mkuu wa umoja huo, Saeed Abu Ali, ameeleza kwamba wajumbe kwenye mkutano wa Jumatano, huko mjini Cairo watajadili njia za kuukabili uamuzi huo.

Wizara ya mambo ya nje ya Uturuki imesema aamuzi wa Marekani kuhamishia ubalozi wake hadi mjini Jerusalem ulihamasisha vikosi vya Israeli kuwaua waandamanaji wa Kipalestina kwenye mpaka wa Gaza na kwamba Uturuki inalaani mauaji hayo yaliyofanywa na maafisa wa usalama wa Israeli.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...