Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Je Ukraine itaenedelea kupokea gesi kutoka Urusi?


Rais wa Urusi Vladimir Putin amemwambia kansela Angela Merkel kwamba gesi ya asili ya Urusi inaweza kupelekwa kwenye nchi jirani ya Ukraine iwapo yatakuwepo manufaa ya kiuchumi kwa Urusi.


Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na rais wa Urusi Vladimir Putin kwenye mazungumzo yao wamejadiliana kuhusu mgogoro wa nchini Ukraine, wakati ambapo Urusi inaongeza ukubwa wa bomba lake la gesi ya asili kwenda moja kwa moja hadi nchini Ujerumani, bila kupitia Ukraine.


Rais Putin na Waziri wake Mkuu Dmitry Medvedev walimkaribisha Kansela Merkel katika makao ya rais ya majira ya kiangazi yaliyopo katika jiji la kusini mwa Urusi la Sochi, kansela Merkel ndiye aliyeongoza vikwazo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Urusi wakati nchi hiyo ilipolitwaa jimbo la Crimea miaka minne iliyopita.


Lakini katika miezi ya hivi karibuni, Ujerumani ilitoa idhini yake kwa Urusi kuweza kutanua bomba lake la gesi la Nord Stream, ambalo litasafirisha gesi ya asili hadi nchini Ujerumani licha ya Ukraine kuupinga mradi huo na kusema kwamba unakiuka vikwazo dhidi ya Urusi. Waziri wa uchumi wa Ujerumani Peter Altmaier, ameitembelea Ukraine mara mbili wiki hii ili kuihakikishia nchi hiyo msaada wa Ujerumani.


Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na rais wa Urusi Vladimir Putin


Mkutano wa viongozi hao unatarajiwa kutoa nafasi mpya ya kujadili mambo mengine na pia Ujerumani na Urusi zote zinataka kuokoa mpango wa nyuklia wa Iran baada ya rais wa Marekani Donald Trump kuiondoa nchi yake kutoka kwenye mpango huo.


Uhusiano wa Ujerumani na Urusi unakabiliwa na vizingiti kadhaa. Kwanza ni kuhusu Mashambulizi ya mtandaoni ambapo Idara ya ujasusi ya nchini Ujerumani inaamini kwamba Urusi inahusika na mashambulizi katika mitandao ya Ujerumani. Kwa mfano mashambulizi dhidi ya mtandao wa Bunge la Ujerumani ya mwaka 2015, pamoja na kwenye mitandao binafsi ya vyama vya kisiasa na pia kwenye wakfu za hapa Ujerumani.


Pia idara ya usalama wa ndani ya nchini Ujerumani, BfV, inaishutumu Urusi kwa kuhusika na shambulio katika mtandao wa serikali ya Ujerumani la mwezi Februari mwaka huu wa 2018 ambapo kiwango kikubwa cha data kiliibiwa.


Mengine ni kuhusu jukumu la Urusi huko nchini Syria, Urusi kulitwaa jimbo la Crimea, tabia ya ushari, maendeleo duni huko mashariki mwa Ukraine, vikwazo vya usafiri na unyanyasaji. Kansela Merkel amesema Urusi lazima ihusishwe katika mchakato wa kutafuta amani nchini Syria.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...