Switzeland imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kusaidia sekta mbalimbali za Maendeleo hususan katika suala la afya, kuongeza ajira na kukuza ujuzi .
Hayo yamebainishwa wakati wa Mkutano uliofanyika Jijini Dodoma kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango na Balozi wa Switzerland nchini, Florence Tinguely Mattli, uliojaili uhusiano kati ya nchi hizo mbili na namna ya kuboresha ushirikiano.
Katika Mkutano huo, Waziri Mpango amemuomba Balozi huyo kuangalia uwezekano wa kuwapa mafunzo madaktari Bingwa nchini ili kukidhi uhitaji uliopo hususan katika Jiji la Dodoma ambalo ndiyo makao Makuu ya Nchi na idadi ya wakazi wake inaongezeka.
Pia amemuomba kufadhili mafunzo kwa watumishi wa umma ili kuwajengea uwezo katika kada mbalimbali lengo likiwa ni kuongeza ufanisi kazini.
Aidha kuhusu suala la uboreshaji miundombinu ya Jiji la Dodoma, Waziri Mpango aliiomba Switzerland kuangalia uwezekano wa kufadhili miradi ya maendeleo katika sekta ya maji na mazingira.
āTanzania ni nchi ya tatu kwa kuwa na mifugo mingi Barani Afrika lakini ufugaji wa mifugo hiyo hauna ubora kwa kuwa Switzerland imeendelea katika Sekta ya Mifugo fursa ipo ya uwekezaji katika eneo hilo nchini,ā alisema Dkt. Mpango.
Amesema kuwa Serikali inafanya jitihada mbalimbali za kukabiliana na umasikini hivyo ni vema washirika wa Maendeleo wakatambua kuwa hatua ambazo Serikali inazichukua zikiwemo za kupambana na wakwepa kodi na kuboresha mikataba zenye lengo la kuboresha maisha ya watanzania kwa kuhakikisha wananufaika na rasilimali nyingi zilizopo nchini na wawekezaji waweze kunufaika pia.
Waziri Mpango amesema kuwa Switzerland inashiriki kikamilifu katika miradi ya Matumizi bora ya misitu hususani mkoani Morogoro, kuboresha ujuzi na kukuza ajira kwa Watanzania.
Kwa upande wake, Balozi wa Switzerland nchini, Florence Tinguely Mattli, amesema kuwa uhusiano kati ya nchi yake na Tanzania umezidi kuimarika na kuahidi kuendelea kuisaidia Tanzania katika sekta mbalimbali za maendeleo huku akisisitiza suala la kuzingatia uwazi na mazingira bora ya uwekezaji kwa kuwa ni chachu kubwa ya kuvutia uwekezaji wenye tija kwa pande zote mbili
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni