Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 15.05.2018


Jonjo Shelvey

Kiungo wa kati wa Newcastle Jonjo Shelvey, 26, hatajumuishwa kwenye kikosi cha Uingereza kitakachoshiriki kombe la dunia kutokana rekodi yake mbaya kinidhamu. (Mirror)


Manchester United wako tayari kuilipa Napoli pauni milioni 44 kumpata beki Elseid Hysaj msimu huu. Raia huyo wa Albania wa umri wa miaka 24 atakuwa mlinzi namba saba ghalia zaidi duniani. (Sun)




Everton watamfuta meneja Sam Allardyce saa 48 zinazokuja na wanakaraibia kumteua aliyekuwa meneja wa Watford Marco Silva. (Mirror)



Sam Allardyce

Afisa mkuu mtendaji wa Arsenal Ivan Gazidis na mkrugeni mkuu Josh Kroenke wamemtambua kiungo wa kati wa zamani wa Arsenal Mikel Arteta ambaye sasa ni kocha huko Manchester City kama mtu anayeweza kuchukua mahala pake Arsene Wenger kama meneja wa Arsenal. (Mail)




Meneja wa Juventus Massimiliano Allegri bado anaweza kuwa meneja wa Arsenal ikiwa atashinda vita vya kuhama wachezaji. (Star)



Arsenal: Pierre-Emerick Aubameyang

Mshambulizi wa Arsenal Pierre-Emerick Aubameyang anasema alijiunga na klabu hiyo akiwa na imani kuwa Wenger atakabaki kama meneja kwa miaka kadhaa. (Evening Standard)


Steve Bould atachelewesha uamuzi ikiwa atabakia au la kama kaimu meneja wa Arsenal, anaposubiri kujua ni nani atakuwa meneja. (Telegraph)




West Ham walikutana na meneja wa Shakhtar Donetsk Paulo Fonseca saa chache baada ya mkataba wa meneja David Moyes kufika mwisho. (Mail)



David Moyes

West Ham watamfuta Moyes na watakuwa na majina matatu kwenye orodha yao. (Teamtalk)


Manchester City wanalenga kumsaini wing'a wa Crystal Palace na Ivory Coast Wilfried Zaha, 25. (Star)



Manchester United wanakumbwa na upinzani kutoka kwa Paris St-Geraon kumsania kiungo wa kati wa Shakhtar Donetsk Fred, 25. (Manchester Evening News)



Rafael Benitez

Meneja wa Newcastle Rafael Benitez anasema hana nia ya kurejea Napoli kwa kuwa yuko kwenye mazungumzo na Magpie kuhusu mkataba mpya. (Calcio Napoli 24 - in Italian)


Benitez amefanya mazungumzo na kipa wa Paris St-Germain Alphonse Areola, 29. (France Football - via Metro)




Real Madrid wako tayari kumwendea kipa Chelsea Thibaut Courtois, 26, wakati mbelgiji huyo akiingia miezi 12 ya mwiso ya mkataba wake.



Thibaut Courtois

Southampton wanataka kumsaini wing'a wa Celta Vigo Pione Sisto, 23. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Denmark ana kipengee cha pauni milioni 36 cha kuondoka mapema kwenye mkataba wake.


Wing'a raia wa Morocco Sofiane Boufal, 24, amezungumzia nia yake ya kurejea ligi ya Ufaransa siku moja tu baada ya kukamilika kwa Premier League.(SFR Sport


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...