MTEULE THE BEST
Uchaguzi Kenya 2017: Mahakama ya Juu kusikiliza kesi muhimu
Mahakama ya juu nchini Kenya leo Jumatano itasikiliza kesi ya dharura iliyowasilishwa na wapiga kura watatu dakika za mwisho wakidai kuwa Kenya haiko tayari kufanya uchaguzi huo.
Mahakama imeombwa kuingilia kati na kuamua - iwapo uchaguzi wa marudio utafanyika..
Wanataka uchaguzi huo uahirishwe.
Rais Uhuru Kenyatta anasema uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa siku ya Alhamisi.
Muungano wa upinzani chini ya kinara Raila Odinga umetaka wafuasi wake wasusie zoezi hilo, ukiutaja kuwa uchaguzi usioweza kuwa wa huru na wa haki.
Odinga amesema Serikali ya Kenya na tume ya Uchaguzi zimeshindwa kushughulikia mapungufu yaliyosababisha mahakama ya juu zaidi nchini humo kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi Agosti.
Uchaguzi Kenya: Tume yasema wagombea wote watashiriki
Kenyatta akutana na mkuu wa uchaguzi Kenya
Kwa nini Roselyn Akombe alijiuzulu IEBC
Hatua hiyo inajiri baada ya mahakama hiyo kufanya uamuzi wa kihistoria ilipofutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais na kutaka uchaguzi huo kurejelewa.
Kuna utata kati ya sheria za uchaguzi, katiba na vile mahakama ilivyofafanua sheria hizo.
Mahakama ya juu imekubali kusikiliza ombi hilo la muda wa lala salama ambalo linahoji iwapo tume ya uchaguzi na mwenyekiti wake wataweza kufanya uchaguzi ulio huru na haki siku ya Alhamisi.
Kumeshuhudiwa maandamano ya wafuasi wa upinzani wanaopinga uchaguzi huo wa marudio na wanashinikiza maguezi ndani ya tume ya uchaguzi IEBC na pia katika mfumo wenyewe wa uchaguzi.
Click to see content: Kenya_provisional_results_ws_swahili
IEBC ilitangaza kwamba Rais Kenyatta alipata kura 8,203,290 ambayo ni asilimia 54.27 naye Bw Odinga akapata kura milioni 6,762,224 ambayo ni asilimia 44.74 katika uchaguzi huo wa tarehe 8 Agosti ambao matokeo yake yalifutwa.
Uchaguzi Kenya 2017: Mahakama ya Juu kusikiliza kesi muhimu
Mahakama ya juu nchini Kenya leo Jumatano itasikiliza kesi ya dharura iliyowasilishwa na wapiga kura watatu dakika za mwisho wakidai kuwa Kenya haiko tayari kufanya uchaguzi huo.
Mahakama imeombwa kuingilia kati na kuamua - iwapo uchaguzi wa marudio utafanyika..
Wanataka uchaguzi huo uahirishwe.
Rais Uhuru Kenyatta anasema uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa siku ya Alhamisi.
Muungano wa upinzani chini ya kinara Raila Odinga umetaka wafuasi wake wasusie zoezi hilo, ukiutaja kuwa uchaguzi usioweza kuwa wa huru na wa haki.
Odinga amesema Serikali ya Kenya na tume ya Uchaguzi zimeshindwa kushughulikia mapungufu yaliyosababisha mahakama ya juu zaidi nchini humo kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi Agosti.
Uchaguzi Kenya: Tume yasema wagombea wote watashiriki
Kenyatta akutana na mkuu wa uchaguzi Kenya
Kwa nini Roselyn Akombe alijiuzulu IEBC
Hatua hiyo inajiri baada ya mahakama hiyo kufanya uamuzi wa kihistoria ilipofutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais na kutaka uchaguzi huo kurejelewa.
Kuna utata kati ya sheria za uchaguzi, katiba na vile mahakama ilivyofafanua sheria hizo.
Mahakama ya juu imekubali kusikiliza ombi hilo la muda wa lala salama ambalo linahoji iwapo tume ya uchaguzi na mwenyekiti wake wataweza kufanya uchaguzi ulio huru na haki siku ya Alhamisi.
Kumeshuhudiwa maandamano ya wafuasi wa upinzani wanaopinga uchaguzi huo wa marudio na wanashinikiza maguezi ndani ya tume ya uchaguzi IEBC na pia katika mfumo wenyewe wa uchaguzi.
Click to see content: Kenya_provisional_results_ws_swahili
IEBC ilitangaza kwamba Rais Kenyatta alipata kura 8,203,290 ambayo ni asilimia 54.27 naye Bw Odinga akapata kura milioni 6,762,224 ambayo ni asilimia 44.74 katika uchaguzi huo wa tarehe 8 Agosti ambao matokeo yake yalifutwa.
Maoni