Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tanzania yawatimua mawakili 3 wa Afrika Kusini kwa ''kukuza mapenzi ya jinsia moja

MTEULE THE BEST''

Tanzania imewafurusha mawakili watatu wa Afrika Kusini waliokamatwa wiki hii wakituhumiwa kwa kukuza mapenzi ya jinsia moja.
Walikuwa miongoni mwa watu 13 waliokamatwa katika hoteli moja mjini Dar es Salaam .
Waandalizi wa mkutano huo wanasema kwamba mkutano huo ulikuwa umeitishwa kujadili iwapo wakabiliane na uamuzi wa serikali ya Tanzania kuzuia utoaji wa baadhi ya huduma za afya.
Majina ya wapenzi wa jinsia moja kutotangazwa hadharani Tanzania
Wapenzi 3 wa jinsia moja watakiwa kuripoti polisi Tanzania
Zaidi ya wanaume 40 wapenzi wa jinsia moja kufikishwa mahakamani Nigeria
Tanzania yasimamisha huduma za vituo 40 vya afya
Mapema mwaka huu, serikali ilipiga marufuku baadhi ya kliniki za kibinafsi kutotoa huduma za ugonjwa wa HIV na ukimwi ikisema zilikuwa zikukuza mapenzi ya jinsia moja ambayo ni haramu nchini Tanzania.
Hatahivyo, Sibongile Ndashe anasema kuwa walikuwa hawana haki ya kuwakamata na ameishtumu mamlaka ya Dar es Salaam kwa kuwakamata yeye na wenzake.
Mapenzi ya jinsia moja ni haramu nchini Tanzania.
Lazaro Mambosasa , afisa mkuu wa polisi mjini Dar es Salaam aliwaambia maripota kabla ya mawakili hao kukamatwa kwamba walikuwa wakikuza mapenzi ya jinsia moja.
Kukamatwa kwao kunajiri kufuatia hotuba ya mwezi Septemba iliotolewa na naibu waziri wa afya Hamis Kingwangala ambaye aliapa mbele ya bunge kukabiliana na makundi yoyote yanayounga mkono wapenzi wa jinsia moja nchini humo, kulingana na chombo cha habari cha AFP.
Lakini bi Ndashe aliambia wanahabari hakuna makosa ambayo wangeshtakiwa nayo kwa kuwa mkutano huo haukuwa wa wapenzi wa jinsia moja .
Shirika la haki za kibinaadamu la Human Rights Watch limesema kuwa kundi hilo linaweza kuishtaki serikali ya Tanzania kwa kupiga marufuku vituo vya afya vinavyowauguza wato waliopo katika hatari ya kuambukizwa ukimwi mbali na uagizaji wa kifaa cha mafuta ambayo yanaweza kutumika kujilinda dhidi ya HIV.
Bi Ndashe anasema kuwa hatua yao ya kutaka kujua sababu za wao kutimuliwa nchini humo hazikuangaziwa.
Kundi hilo sasa limeonya kwenda mahakamani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...