Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Raila Odinga akana kuitisha maandamano siku ya uchaguzi

MTEULE THE BEST

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amewataka wafuasi wake kutoandamana na badala yake kusalia majumbani mwao siku ya uchaguzi.
''Hatujawaambia watu wafanye maandamano siku ya uchaguzi. Hatujasema hilo hata kidogo'', Odinga alisema siku ya Jumanne katika mahojiano na BBC.
Alhamisi iliopita , Bwana Odinga na upinzani wake wa Nasa uliwaambia wafuasi wao kujiandaa kufanya maandamano wiki ya Uchaguzi mkuu.
Odinga akosa kutangaza mwelekeo Kenya
Afisa mkuu wa tume ya uchaguzi Kenya ajiondoa
Upinzani Kenya wadai Odinga ndiye mshindi wa urais
Lakini katika mahojiano, bwana Odinga alisema kuwa maoni yake ni tofauti na yale ya rais Uhuru Kenyatta ambaye amesisitiza kwamba ni lazima uchaguzi ufanyike katika kipindi cha siku 60 kama ilivyoagizwa na mahakama ya juu.
''Kuna kambi mbili hapa, wale ambao wanataka kushiriki katika uchaguzi usio huru na haki na wale ambao wanasema hapana sio sawa kufanya hivyo'', alisema Odinga.
Baada ya Raila Odinga kushinda katika malalamishi yake aliyoiwasilisha mahakamani , tume ya uchaguzi ilichapisha tarahe 26 kuwa tarahe ya uchaguzi mpya baada ya mahakama ya juu kufutilia mbali ushindi wa rais Uhuru Kenyatta.
Lakini bwana Odinga aliwasilisha orodha ya masharti kwa tume ya uchaguzi ambayo alisema ni sharti yaafikiwe kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mpya ikiwemo kubadilishwa kwa kampuni itakayochapisha makaratasi ya kupigia kura, kampuni yenye mfumo wa kielektroniki ya kupigia kura, mbali na kushinikizwa kujiuzulu kwa afisa mkuu wa tume hiyo Ezra Chiloba pamoja na maafisa wengine wakuu wa tujme hiyo.
Wiki mbili kabla ya uchaguzi , bwana Odinga alijiondoa katika uchaguzi huo na kutaka uchaguzi mpya kufanyika baada ya siku 90 baada ya uteuzi kufanywa.
Kamishna wa tume ya uchaguzi Kenya akimbilia Marekani
Wanaharakati washutumu mauaji ya meneja wa tume ya uchaguzi Kenya
Tume ya uchaguzi Kenya yapokea karatasi za kura ya urais
Lakini uamuzi wa mahakama kuu uliowaruhusu wagombea wengine wanane kushiriki katika uchaguzi huo ulimrudisha rais Odinga katika wagombea wanaofaa kushiriki katika uchaguzi, huku rais Uhuru Kenyatta akisema kuwa ni chaguo la Odinga kushiriki uchaguzi huo au la.
Katika mahojiano hayo bwana Odinga amelitaja kama jaribio la kuwatishia Wakenya hatua ya vigogo wa chama tawala cha Jubilee kuvalia magwanda ya kijeshi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...