Raia mmoja wa Korea Kaskazini amemuomba rais wa China Xi Jinping kutomrudisha nyumbani mkewe na mwanawe wa kiume akisema kuwa watakabiliwa na kifungo jela au kifo iwapo watarudishwa Korea Kaskazini.
Mwanamke na mvulana wa miaka minne wanaeleweka kuwa miongoni mwa kundi la watu 10 wa Korea Kaskazini waliozuiliwa nchini China wiki iliopita baada ya kuvuka na kuingia nchini humo kisiri.
Mtu huyo ambaye alitaka kutambulika kwa jina la Lee pekee , alitorokea Korea Kusini 2015.
Alirekodi ombi lake katika mkanda wa video ambao uliwasilishwa kwa BBC.
Alisema kuwa mkewe na mwanawe watakabiliwa na hatia ya kifo ama kufungwa jela iwapo watarudishwa nyumbani Korea Kaskazini.
''Ningependa rais Xi Jinping na rais Donald Trump kumfikiria mwanangu kama kilembwekeza wao na kumleta mwanangu katika taifa huru la Korea Kusini '', alisema.tafadhali tusaidie.
''Okoa familia yangu kutorudishwa Korea Kaskazini. Mimi kama baba nawaomba viongozi hawa wawili kuisaidia familia yangu. Tafadhalini tusaidieni.Anasema kuwa anafuatwa na kiwiliwili cha mwanaye katika jela''.
''Nasikia sauti ya mwanangu ikiniita'', alisema.
''Namuona mwanangu katika jela ile baridi akimlilia babake, alisema.
''siwezi kusimama na kutochukua hatua yoyote''
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni