Wanasayansi nchini Uingereza wamegundua kwamba majeraha ya kukatwa na kuchomeka hupona haraka yanapopatikana mchana ikilinganishwa usiku.
Wanasema kwamba ni kutokana na mwili unavyohisi kulingana na muda.
Utafiti huo unasema kuwa seli za ngozi ya mwanadamu hubadilisha tabia yake kulingana na muda huku protini zinazohitajika kurekebisha majeraha hayo zikifanya kazi vizuri wakati wa mchana.
Jeraha la kuchomeka nyakati za usiku lilichukua siku 28 kupona ikilinganishwa na siku 17 za jereha la wakati wa mchana.
Watafiti walitaja tofauti hiyo kuwa kubwa huku wakiongezea kwamba wanaweza kuharakisha watu kupona kwa kutumia dawa za steroids ambazo hubadilisha muda wa mwili.Utafiti: Mbwa mwitu hufanya uamuzi kwa kupiga chafya
Utafiti uliochapishwa katika jarida la Sayansi uliwahoji wagonjwa 118 katika kitengo cha wagonjwa waliochomeka nchini Uingereza.
Ulionyesha muda wa kupona wa 11 kati ya watu nyakati za mchgana na usiku.
Matokeo ya mahabara yalionyesha kuwa seli za ngozi kwa jina Fibroblast zilikuwa zikibadili uwezo wake katika kipindi cha saa 24.
Seli hizo ndizo za kwanza zinazokimbia katika jeraha hilo ili kufunga kidonda.
Nyakati za mchana huwa zinafanya kazi sana na hupoteza nguvu hiyo nyakati za usiku.
Daktari O'neil mmoja ya watafiti aliambia BBC ''ni kama kukimbia mita 100''. Mkimbiaji hujiandaa kutoka , kawaida atamshinda yule aliyesimama akijiandaa kukimbia''.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni