Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 30.04.2018

Mkufunzi mkuu wa Real Madrid Zinedine Zidane amesema washambuliaji wake Gareth Bale, 28, na Karim Benzema, 30, "watasalia" katika klabu hiyo licha ya tetesi kudokeza kwamba huenda wakahama. (Star)


Bournemouth wanaaminika kuwa tayari kushindana na Tottenham na Manchester United katika kutafuta saini ya beki wa Celtic kutoka Scotland Kieran Tierney, 20. (Sun)


Meneja wa Arsenal anayeondoka Arsene Wenger atachukua "miezi minne hadi mitano" kuamua kuhusu mustakabali wake. (London Evening Standard)



Mshambuliaji wa zamani wa Celtic Chris Sutton anasema "litakuwa jambo zuri sana kwa soka ya Scotland iwapo Steven Gerrard atakuwa meneja wa Rangers". Hata hivyo amemtahadharisha nahodha huyo wa zamani wa Liverpool kwamba "hatua kama hiyo inaweza kufuta matumaini yake ya kuwa mkufunzi tajika hata kabla yake kuanza" (Mail)


Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino amekataa kuthibitisha iwapo atakuwa kwenye klabu hiyo msimu ujao. (Mirror)


Naye meneja msaidizi wa Liverpool Zeljko Buvac ameihama klabu hiyo baada ya kuzozana na meneja wa sasa Jurgen Klopp. (Daily Record)


Mshambuliaji wa Crystal Palace mwenye miaka 27 Christian Benteke, ambaye amesalia na miaka miwili pekee katika mkataba wake na klabu hiyo, amesema atajadiliana kuhusu hatima yake na klabu hiyo mwisho wa msimu. (Mail)


Mfanyabiashara Mmarekani Shahid Khan anaweza akaukubali mpangilio wa "lipia ukiendelea kuchezea" kati yake na Chama cha Soka cha England kama sehemu ya makubaliano kati yake na chama hicho kuhusu ununuzi wa uwanja wa Wembley. Mpangilio kama huu unaweza kuifanya nafuu kwa FA kutumia viwanja vya nje kucheza mechi zake. (Times )


Klabu ya West Brom ambayo imo hatarini ya kushushwa daraja itapigania kusalia na beki wa England Craig Dawson mwenye miaka 27 ambaye anatafutwa na Burnley, Wolves na West Ham. (Mirror)


Kipa wa West Brom Ben Foster, 35, amesema kaimu meneja wao Darren Moore amefanikiwa kurejesha tena umoja katika timu hiyo na angependa mkufunzi huyo amepewe kazi hiyo kwa mkataba wa kudumu. (Telegraph)


Meneja wa Chelsea Antonio Conte amesema matatizo ambayo yameikumba timu hiyo msimu huu ni kutokana na kutomakinika vyema zaidi kwenye goli. (Express)




Meneja wa Manchester City Pep Guardiola ametania kwamba mabingwa hao wa Ligi ya Premia wanaweza kutumia £1bn kipindi cha kuhama wachezaji mwisho wa msimu. (ESPN)


Guardiola amesema Manchester City hawatasaini wachezaji zaidi ya wawili mwisho wa msimu. (Manchester Evening News)


Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ana wasiwasi kwamba huenda mshambuliaji wake Romelu Lukaku, 24, huenda asiweze kucheza fainali ya Kombe la FA dhidi ya Chelsea baada yake kuumia mguuni akicheza dhidi ya Arsenal Jumapili. (Times )


Ajax wanamtaka kinda wa miaka 19 wa Chelsea anayecheza safu ya kati Mason Mount. Mount alikuwa kwenye kikosi cha England kilichoshinda ubingwa wa Ulaya kwa wachezaji wa chini ya miaka 19 mwaka jana. (Sun)


Wolves wamewaomba radhi mashabiki wao baada ya kusahau kuandaa gwaride la kusherehekea kushinda ligi ya Championship Jumamosi. (Birmingham Mail)




Wachezaji wa Newcastle hatimaye walipata fursa ya kushiriki sherehe yao ya Krismasi mwishoni mwa wiki. (Newcastle Chronicle)


Mkufunzi mkuu wa Watford Javi Gracia amesema ana imani kikamilifu na watabibu wa timu hiyo licha ya kutokea kwa msururu wa visa vya wachezaji wa klabu hiyo ya Vicarage Road kuumia. (Watford Observer)


Meneja wa Leicester City Claude Puel amesema pengine wachezaji wameanza kuleweshwa na Kombe la Dunia au mambo mengine baada ya uchezaji wa timu yake kudorora. Walichapwa 5-0 na Crystal Palace. (Guardian)



Claude Puel

Mpenzi wa mchezaji wa zamani wa Newcastle Davide Santon amesema ana wasiwasi kuhusu kukaa kwao nyumbani baada yake na beki huyo wa Inter Milan kutumiwa ujumbe wa vitisho. (Football Italia)




Brighton wanatarajiwa kukoleza ushirikiano na Gereza la Lewes kama sehemu ya mpango wa kuwasaidia wafungwa kuzoea maisha ya kawaida baada ya kuachiliwa huru. (Argus


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...