Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 08.04.2019: Pochettino, Pogba, Kepa, Giroud, Coutinho


Philippe Coutinho

Winga wa zamani wa Liverpool Philippe Coutinho - ambaye kwa sasa yupo Barcelona ya Uhispania- anasema hana mpango wa kurejea kwenye ligi ya Premia. Coutinho, 26, ambaye ni nyota pia wa timu ya taifa ya Brazil alijiunga na Barca Januari 2018. (Mirror)

Real Madrid wanatarajiwa kutangaza dau la kumnunua kipa wa Chelsea raia wa Uhispania Kepa Arrizabalaga, 24. (Teamtalk)

Chelsea wanataka kumsajili kiungo wa klabu ya Athletico Paranaense ya nchini Brazil Bruno Guimaraes, 21, iwapo watafamikiwa kuchomoka kwenye marufuku ya kufanya usajili. (Mail)


Real Madrid wanamatumaini kuwa wakala Mino Raiola atamshawishi mchezaji wake Paul Pogba, 26, ahamie timu yao kutoka Manchester United. (Marca)

AC Milan wanamtaka kocha wa Tottenham Mauricio Pochettino kumrithi Gennaro Gattuso kushika mikoba ya timu hiyo na watampatia kitita cha pauni milioni ili afanye usajili wa wachezaji mwishoni mwa msimu huu. (Mirror)


Kablya ya kutua Spurs, Mauricio Pochettino alikuwa meneja wa Espanyol kati ya 2009 na 2012.

Liverpool wapo tayari kumpa mkataba mpya mshambuliaji raia wa Ubelgiji Divock Origi, 23. (Football Insider)

Kocha wa Chelsea Maurizio Sarri anaamini kuwa mshambuliaji wake raia wa Ufaransa Olivier Giroud, 32, ataendelea kusalia klabuni hapo msimu ujao. (Mail)


Kocha wa Chelsea Maurizio Sarri

Kocha wa West Ham Manuel Pellegrini anataka kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Roma na timu ya taifa ya Bosnia Edin Dzeko, 33. (Express)

Kipa wa zamani wa taifa la Uholanzi Edwin van der Sar amesema "siku moja" anaweza kurejea Manchester United. Mkongwe huyo mwenye miaka 48, kwa sasa ni mkurugenzi wa mpira wa miguu kwenye klabu ya Ajax, na enzi zake aliichezea United kwa misimu sita. (Times - subscription required

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...