Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mamlaka nchini Kenya zawazuia marubani wanafunzi kutua nchini humo



Marubani wanafunzi wa Afrika Kusini, waliotengeneza ndege aina ya Sling 4, wamewasili Kilimanjaro,Tanzania, wakiwa njiani kuelekea kwenye kituo chao cha mwisho, jijini Cairo.


Timu ya wanafunzi hao waliondoka Zanzibar siku ya Jumapili, baada ya kutumia siku kadhaa bila mafanikio kuzungumza na mamlaka za nchini Kenya ili waweze kutua jijini Nairobi.

''Mamlaka nchini Kenya wamesema hawajafurahishwa na njia zetu hivyo wakatuzuia kuingia,'' alisema kiongozi wa wanafunzi hao, Des Werner, Baba wa Megan Werner 17, mwanzilishi waU-Dream Global.

''Tunaweza kubadili njia lakini hatuna muda wa kufanya hivyo.Tunafikiri kama ni wagumu tusilazimishe kwenda. Hata hivyo ni nchi yao ndio inayokosa nafasi ya vijana wa nchini kwao kuzungumza na timu yetu kwa ajili ya kuwapa msukumo vijana wa nchini mwao.''

Ndege iliyotengenezwa na wanafunzi yatua Zanzibar

Wanafunzi kuendesha ndege kutoka Afrika Kusini mpaka Misri

Marubani hao wataelekea Uganda siku ya Jumanne lakini bado wanasubiri kibali cha kuruka mpaka Addis Ababa, safari ambayo iko kwenye mipango yao.

''Kidogo tuko nyuma ya ratiba lakini tutafanikisha.Kama mambo yakiwa sawa tunatarajia kuwa Cairo tarehe 7 mwezi Julai,'' ameeleza bwana Werner.

Wanafunzi hao wanaendesha ndege mbili aina ya sling 4 yenye viti vinne, ndege moja inayorushwa na marubani wadogo ambao wamekuwa wakibadilishana tangu walipotoka Cape Town tarehe 15 mwezi Juni na nyingine iliyoendeshwa na timu ya watu wenye uzoefu.

Bwana Werene, amesema timu yake wako na ari na kuwa hali ya safari kwa ujumla ni nzuri.

Ndege ilitengenezwa vipi?

Wanafunzi hao waliitengeneza ndege hiyo katika kipindi cha wiki tatu, wakiunganisha vifaa vilivyonunulia kwenye kampuni moja nchini Afrika Kusini.

"Nikiiangalia hii ndege, huwa ninaona fahari ya hali ya juu kwa kile nilichokifanya. Siamini kile tulichokifanya. Ninaiona kama mtoto wangu. Ninamtukuza mtoto (ndege)," ameeleza Agnes Keamogetswe Seemela, msichana kutoka katika jimbo la Gauteng mwenye umri wa miaka 15.

"Inapaa uzuri kabisa, na ukiwa juu, mwonekano wa chini ni mzuri kweli," ameeleza kulingana na safari ya kwanza ya ndege hiyo kutoka jiji la Johannesburg mpaka Cape Town, kabla ya kuanza safari ya Misri.

"Nilishiriki katika kuunda eneo la kti la ndege hiyo pamoja na mabawa yake."

Safari inaendelea

Vituo ambavyo ndege hiyo itasimama kutoka Afrika Kusini mpaka Misri.

Kitua cha kwanza cha safari hiyo ni mji wa kusini katika pwani ya Namibia wa Luderitz, na tayari wameshatua huko.

Ndege hiyo ina uwezo wa kupaa angani kwa muda wa saa sita na nusu, na itakuwa na vituo kadhaa katika nchi za Zimbabwe, Malawi, Tanzania, Kenya, Ethipia na Eritrea kabla ya kufika Misri.

Katika safari ya kurudi, watatumia njia tofauti na watasimama katika nchi za Uganda, Rwanda, Zambia na Botswana.

Kutakuwa na ndege nyengine aina ya Sling 4 pkwa ajili ya usaidizi.

Marubani hao wanafunzi wanapanga kuzungumza na wanafunzi wenzao katika nchi zote ambazo watasimama.

"Ni kitu kizuri kuona ni kwa namna gani watu wanavutia na kushawishika na kile ambacho tumefanya," amesema rubani Megan

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...