Ruka hadi kwenye maudhui makuu

setilaiti ya juno yafika jupiter

MTEULE THE BEST

 

 

Ile Setilaiti ya Juno iliiyosafiri kwa miaka mitano kwenda katika sayari ya Jupiter imefika kwenye sayari hiyo na kuanza kuizunguka.
Wanasayansi wanakadiria setilaiti hiyo ilifika muda mfupi ujao majira ya saa 12:15 asubuhi hii kwa saa za Afrika Mashariki.
Setilaiti hiyo inatarajiwa kudumu kwa mwaka mmoja na nusu kuchunguza sayari jinsi ilivyoumbwa.
Mawasiliano kutoka kwa chombo hicho cha juu yalipokelewa katika maabara ya Nasa eneo la Pasadena, California kwa shangwe.
"Vituo vyote vya Juno, tunapokea sauti ya kufanikiwa kwa chombo Delta B," kituo cha udhibiti wa Juno kilitangaza. "Roger Juno, karibu Jupiter."


Chombo cha Juno kikipaa
Wanasayansi wanatarajiwa kutumia chombo hicho kufahamu Zaidi muundo wa sayari ya Jupiter ambayo hujulikana kwa Kiswahili kama Zohali.
Wanafikiri muundo wake kikemia unaweza kutoa ufahamu kuhusu jinsi sayari hiyo iliundwa miaka bilioni nne unusu iliyopita.
Hakuna chombo cha anga za juu kilichowahi kufika karibu sana na sayari hiyo kama kilivyofanya chombo cha Juno.
Miali nururishi kutoka kwa sayari hiyo huwa na uwezo wa kuharibu vyombo vya kielektroniki visivyokingwa vyema.
Chombo vya Juno kimezingirwa na kinga ya madini ya Titanium.
Kwa sasa Juno itakuwa ikichukua siku 53 kuizunguka sayari hiyo.
Baadaye Oktoba, itaongeza kasi na kuikaribia zaidi sayari hiyo na kuanza kutumia siku 14 kumaliza mzunguko.

Lengo kuu litakuwa kubaini iwapo kuna oksijeni katika sayari hiyo. Hii sana itakuwa imefungamanishwa na maji, iwapo yapo.
"Kiwango cha maji katika sayari ya Jupiter kitatueleza mengi kuhusu ni wapo sayari hiyo ilikuwa ilipoundwa mapema katika mfumo wa jua,ā€ anasema mmoja wa wanasayansi wanaohusika katika mradi huo Candy Hansen.
"Tunafikiri kwamba Jupiter iliundwa ikiwa pahala tofauti na ilipo sasa."
Jupiter ina ukubwa mara 11 kuzidi Dunia na uzito wake ni mara 300 zaidi
Sayari hiyo hutumia miaka 12 ya dunia kulizunguka jua; siku moja huko hudumu saa 10.
Muundo wake ni kama wa nyota , sana haidrojeni na helium.

Nasa inapanga kuitumia Juno hadi Februari 2018.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...