Ruka hadi kwenye maudhui makuu

USIA WA BABA KWA BINTI YAKE ANAEOLEWA.

MTEULE THE BEST

 



USIA WA BABA KWA BINTI YAKE ANAEOLEWA.
1.Mwanangu unakwenda kuolewa na Mwanaume (Mume) na siyo marafiki, Hakikisha haushindi kwa Marafiki sasa kama ilivyokuwa kabla ya kuolewa kwako,Umesikia Mwanangu.....Heshimu ndoa yako
2.Mwanangu SIRI ZAKO NA MUMEWE ni MARUFUKU kuzitoa nje,Usifikiri kila unayemuelezea SIRI Zako na Mumewe anafurahia WENGINE wanakucheka,JIFUNZE KUTUNZA SIRI ZAKO NA MUMEO..Mwanangu
3.Mwanangu Wewe ni Mlinzi wa MUMEO...Mlinde kwa MAOMBI Kila WAKATI Usifikiri MAOMBI YAMEISHA ULIPOINGIA KWENYE NDOA,HAPANA UKIZUBAA TU,YULE MWIZI ATAKUJA (Yohana 10:10)
4.Mwanangu Mimi na Mama Yako tumezeeka na mda wetu umetutupa mkono ila furaha yetu inaenda kutimia kwa kukulea, ukakua katika maadili na ndoa yetu sasa na wewe unaenda kupata yako tumetimiza ndoto yetu ya kukuona ukiwa mama ambaye atayaenzi yote mema na kuwa na ndoa itakayodumu kama yetu ikitawaliwa na furaha na upendo... Linda sana ndoa yako
5. Mwanangu ulipokua mdogo shuleni na nyumbani tulikusifu sana kuwa umechangamka na wajua kuongea kweli kweli tena umerithi kutoka kwa bibi yako ila mwanangu mdomo ule umezibwa rasmi leo yakupasa kuwa na maneno machache au ukimya kabisa maana katika ndoa uongeaji saaaaana ni kero kubwa .... Cha msingi msikilize mmeo.
6. Mwanangu leo unaolewa na mmeo mtakayeishi pamoja milele sio mwanasiasa au mshindani wa debate shuleni tafadhali epuka argument au mabishano yasiyo na msingi ili kujenga familia yenye furaha muda wote... mabishano ni sumu katika ndoa.
7. Mwanangu unaolewa, kule unakoenda kuishi tambua sio kituo cha redio au television bali ni nyumbani kwako wewe na familia yako hivyo ni marufuku kupokea au kusambaza habari za ndani na nje... Epuka umbea ni uchafu katika ndoa.
8. Mwanangu siku ulipojisikia kuumwa au shida yeyote mtu wa kwanza kumshirikisha alikua mama yako kisha baadae mimi, hakika ulifanya vyema kabisa ila sasa mwanangu kuanzia leo ikitokea jambo lolote mtu wa kwanza kumshirikisha awe mme wako.... muamini mmeo.
9. Mwanangu tumekufunza yote ila hatujakufunza mafunzo ya kivita na uasi tafadhali tambua kule unakoenda kuishi mmeo ana wazazi na ndugu zake, waheshimu kama ulivyokua unatuheshimu dumisha upendo tambua wao sasa ndio familia yako mpya.... Epuka kuwa mchochezi na chanzo cha migogoro na chuki NDOA ISIJEKUKUSHINDA.
10. Mwanangu siku zote amini chochote apatacho mtu ni majaliwa ya MUNGU usitamani maisha ya wengine, mvumilie mmeo kwa chochote alichonacho au apatacho, ridhika nae, mkumbatie mtie moyo muombee hakika mtafanikiwa ardhini na mbinguni maana MUNGU hujibu maombi yao wamtafutao kwa bidii wakizishika amri zake na kujituma katika kufanya kazi.. Epuka tamaa ya utajiri na mali nyingi.
Funzo:
Ndoa sio kitchen party au send off bali ni mfumo mpya wa maisha unaohitaji wawili wenye kutoka familia tofauti kuunda familia moja itakayounganisha na kuyaenzi yale yote mema ya pande zote na kuwa bora zaidi itakayodumu kwa mafanikio na amani pia furaha tele.
Kama umeipenda SHARE na marafiki zako

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...