Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Charlottesville: Trump ashutumiwa kuhusu mkutano wa Wazungu wababe

MTEULE THE BEST

Mamia ya Wazungu watetezi wa ubabe, Wanazi mambo leo na watu wa mrengo wa kulia walikabiliana na waandamanaji waliopinga mkutano Charlottesville - 13 AugustHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMamia ya Wazungu watetezi wa ubabe, Wanazi mambo leo na watu wa mrengo wa kulia walikabiliana na waandamanaji waliopinga mkutano Charlottesville
Rais wa Marekani Donald Trump ameshutumiwa vikali kutokana na alivyojibu ghasia zilizozuka katika mkutano wa watetezi wa ubabe wa Wazungu nchini Marekani.
Mwanamke mmoja aliuawa na watu wengine 19 wakajeruhiwa baada ya gari kuvurumishwa kwenye waandamanaji wa kupinga mkutano huo uliofanyika Charlottesville, Virginia.
Bw Trump alishutumu ghasia za "pande nyingi" - lakini hakushutumu moja kwa moja watu wa mrengo wa kulia walioandaa mkutano huo.
seneta wa Republican Cory Gardner amesema "Bwana Rais - ni lazima tuutaje uovu kwa jina lake."
Aliongeza: "Hawa walikuwa wanatetea ubabe wa Wazungu na huu ni ugaidi wa ndani."
Matamshi yake yaliungwa mkono na maafisa wengine wakuu wa chama cha Republican chake Rais Trump.
Mamia ya watu wanaotetea ubabe wa Wazungu walikusanyika kwa maandamano hayo ya Jumamosi yaliyopewa jina "United the Right" (Unganisha mrengo wa Kulia). Walikuwa wanapinga kuondolewa kwa sanamu ya shujaa mtetezi wa kujitenga kwa majimbo ya kusini.
Waandamanaji hao waliojumuisha pia makundi yanayounga siasa za ki-Nazi na wanachama wa Ku Klux Klan, walikabiliana na waandamanaji waliokuwa wanapinga mkutano huo.
Watu walipigana kwa mangumi na mateke, huku gesi ya pilipili ya kuwasha ikitumiwa na pande zote mbili.
Mkutano huo ulipokuwa unakomeshwa, gari lilivurumishwa kwenye waandamanaji wa kupinga mkutano huo.
Gari hilo liliwagonga na kuwarusha watu juu.
Kijana James Fields wa miaka 21 kutoka jimbo la Ohio, ambaye anadaiwa kwua dereva wa gari hilo, amekamatwa na kuzuiliwa kwa tuhuma za kutekeleza mauaji ya ngazi ya pili.
Maafisa wa FBI wameanzisha uchunguzi.
Kando na mauti na majeruhi kutokana na kisa hicho cha gari, polisi wa Charlottesville wamesema watu wengine zaidi ya 15 walijeruhiwa katika ghasia zilizohusiana na maandamano hayo.
Gavana wa Virginia, Terry McAuliffe, alisema ujumbe wake pekee kwa Wazungu wababe waliokuwa wamefika Charlottesville ni kwamba "Waende nyumbani kwao".
White nationalist protest in Charlottesville
A far-right protester clutches a black shieldHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMwandamanaji wa mrengo wa kulia akiwa na ngao ya kujikinga

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...