Usain Bolt aumia na kushindwa mbio zake za mwisho mashindano ya dunia ya IAAF
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST
Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionUsain Bolt ameshinda dhahabu 11 mashindano ya ubingwa wa dunia
Usain Bolt aliumia na kushindwa kumaliza mbio zake za mwisho za ubingwa wa dunia jijini London, na mwanariadha mwenzake Yohan Blake anasema huenda kucheleweshwa kwa mbio hizo kulimwathiri.
Bolt alipata mkakamao wa misuli na kulazimika kuondoka uwanjani alipokuwa akikimbia mbio za kupokezana vijiti za 4x100m ambazo timu ya Uingereza ilishinda.
Yohan Blake alisema hilo: "Mbio zilicheleweshwa dakika 10, tuliwekwa tukisubiri kwa dakika 40. Ilitushangaza sana.
"Watuweka muda mrefu sana tukisubiri."
Bolt alikuwa ametumai kwamba angemaliza maisha yake ya ukimbiaji kwa kushinda dhahabu mbili mashindano hayo ya London lakini ameondoka sasa na nishani ya shaba pekee aliyoishinda kwenye mbio za mita 100 wikendi iliyopita.
Sekunde chache baada yake kupokezwa kijiti awamu ya mwisho ya mbio hizo, alitatizima na kuanguka sakafuni.
Daktari wa timu ya Jamaica Kevin Jones amethibitisha kwamba Bolt alipatwa na mkakamao wa misuli ya mguu wake wa kushoto.
"Ilikuwa dakika 40 na walitoa nishani kwa washindi wa mbio mbili kabla yetu kukimbia," aliongeza bingwa wa zamani wa mbio za mita 100 Blake.
"Tulikaa tukipasha misuli joto na kusubiri, kisha tunapasha misuli moto tena na kusubiri. Nadhani hilo lilitwathiri.
"Inauma kumuona jagina halisi, bingwa halisi akiingia uwanjani na kutatizika kwa namna hiyo."
Bingwa wa mbio za 110m za kuruka viunzi Omar McLeod, aliyeongoza timu ya Jamaica ambayo ilikuwa imeshinda ubingwa wa mbio za 4x100m katika makala manne yaliyopita ya ubingwa wa dunia, alikubaliana na mtazamo wa Blake.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Sherehe za kumuaga Mo Farah baada yake kumaliza nafasi ya pili mbio za 5000m zilionekana kuchelewesha ratiba, na pia Farah alikabidhiwa nishani yake kabla ya fainali ya mbio hizo za kupokezana vijiti.
"Inauma sana. Nilijitolea kabisa na nilitaka sana kumuona Usain akiondoka kwa ushindi, au hata kama ingekuwa nishani tu. Inashangaza bwana, tulisubiri muda mrefu. Nilikunywa chupa mbili za maji.
"Lakini jina la Usain Bolt litasalia kukumbukwa."
Mshindi wa mbio za 100m Justin Gatlin alisema Bolt 'ndiye bado bora zaidi duniani' baada yake kushinda nishani ya fedha na timu yake ya Marekani.
Haki miliki ya pichaEPAImage captionUsain Bolt alikosa kushinda dhahabu mashindano ya ubingwa wa dunia mara ya mwisho 2007
Alikiri kwamba huenda hali ya hewa ilimwathiri Bolt.
"Nafikiri ni hali ya hewa iliyomsababishia Bolt jeraha. Lakini bado ndiye bora zaidi duniani. Huu ni wakati wa kuaga, naanza kumkosa tayari. Sehemu ya kupashia misuli moto, huwa tunaheshimiana na tulisalimiana. Usain Bolt ni mwanariadha mzuri sana."
Haki miliki ya pichaREX FEATURESImage captionBolt (wa nne kutoka kulia) alipokuwa anaumia
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni