Mamia ya wamaasai wapoteza makao Tanzania

MTEULE THE BEST

A Maasai woman holds a sign that reads in Swahili: "We will fight for our land until the end"Haki miliki ya pichaJASON PATINKIN
Image captionKijana mmoja wa kimasai anaripotiwa kupigwa risasi na kujeruhiwa vibaya.
Zaidi ya manyatta 100 za jamii ya Maasai zinadaiwa kuchomwa moto na mamlaka za mbuga ya wanyama pori karibu na mbuga ya wanyama pori ya Serenegeti.
Mamia wa watu wanaripotiwa kubaki bila makao kutokana na kuondolewa kwa jamii hii ya wafugaji.
Kijana mmoja wa kimasai anaripotiwa kupigwa risasi na kujeruhiwa vibaya.
Hii ni sehemu ya mzozo wa muda mrefu kati ya jamii ya Maasai na mamlaka ambazo huendesha shughuli za uwindaji kwa watalii.
Serikali ya Tanzania ina mipango ya kubuni eneo la ukubwa wa kilomita 1500 mraba kwenye mbuga hiyo, kwa kampuni yenye makao yake nchini Dubai ambayo hutoa huduma za uwindaji kwa watalii matajiri kutoka Milki ya nchi za kiarabu.
Maasai cattle herder, Parakapooni, and his brother and son look over the brown plains of the Serengeti, Tanzania.
Image captionKijana mmoja wa kimasai anaripotiwa kupigwa risasi na kujeruhiwa vibaya.
Mipango hiyo itasababisha watu 30,000 kupoteza makao na matatizo mengine kwa jamii ya Masai ambayo hutegemea malisho kwa mifugo wao.
Mwenyekiti wa kijiji cha Ololosokwani Kerry Dukunyi ameambia BBC kuwa wanavijiji wamepoteza mali katika kisa hiki cha hivi punde.
"Kiwango kikubwa cha chakula chetu kimeharibiwa.Tumepoteza chakula kingi," alisema
"Mifugo kadhaa pia hawajulikani waliko."

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU