Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mwanamke ajishindia $758m kwenye jackpot Marekani

MTEULE THE BEST


Mavis Wanczyk
Mshindi wa pesa nyingi zaidi kuwahi kujishindiwa na mtu binafsi katika shindano la bahati nasibu Amerika Kaskazini - jumla ya $758.7m (Ā£590m) - amejitokeza kuchukua zawadi yake, na ni mwanamke.
Mavis Wanczyk, 53, mama wa watoto wawili, alinunua tiketi yake ya ushindi katika kituo cha mafuta Chicopee, Massachusetts.
Mshindi huyo, ambaye namba zake za bahati zilikuwa 6, 7, 16, 23 na 26, na 4 - ameambia wanahabari kwamba tayari ameacha kazi.
Zawadi ya juu zaidi ya jackpot katika shindano la bahati nasibu ya kampuni ya US Powerball kuwahi kutolewa ilikuwa $1.6bn, lakini ilienda kwa washindi watatu ambao waligawana pesa hizo Januari 2016.
Wasimamizi wa mashindano ya bahati nasibu jimbo la Massachusetts waliambia wanahabari kwamba tiketi ya mwanamke huyo ambayo ilishinda Jumatano imethibitishwa kuwa halisi.
"jambo ninalotaka kufanya kwa sasa ni kuketi na ktuulia," alisema Bi lWanczyk.
Pride petrol station in the city of ChicopeeHaki miliki ya pichaWBZ-TV)
Image captionTiketi ya ushindi ilinunuliwa katika kituo hiki cha mafuta Chicopee, Massachusetts
"Ni ndoto kuu ambayo imetimia."
Amewaambia wanahabari kwamba alichagua namba zake kwa kutumia tarehe za kuzaliwa za jamaa zake.
Bi Wanczyk, kuhusu kazi yake aliyoifanya kwa miaka 32 katika kituo cha matibabu, amesema: "Niliwapigia simu na kuwaambia sitafika tena kazini."
Aliongeza kwamba "nitaenda na kujificha kitandani mwangu".
Waandishi walimwuliza iwapo anapanga kujizawadi kwa vitu vizuri, mfano gari la kifahari.
Lakini Bi Wanczyk amejibu kwamba alinunua gari jipya chini ya mwaka mmoja uliopia, kwa mkopo, na sasa anapanga kulipa kiasi kilichosalia.
Afisa mmoja wa mashindano ya bahati nasibu laimweleza mwanamke huyo kama "mkazi wa kawaida sana wa Massachusetts".
Watu wakisubiri kununua tiketi za bahati nasibu Hawthorne, CaliforniaHaki miliki ya pichaEPA
Image captionWatu wakisubiri kununua tiketi za bahati nasibu Hawthorne, California
Aliongeza kwamba anaonekana kama mwanamke mwenye bidii sana na kwamba bila shaka ana furaha isiyo na kifani.
Mwenye kituo cha petroli cha Pride, kilichopokea zawadi ya $50,000 inayotolewa kwa duka linalouza tiketi ya ushindi Bob Bolbuc amesema atatoa pesa hizo kwa hisani.
Malipo ya zawadi hiyo ya Jackpot, ambayo yanaweza kufanywa kwa awamu mara 29 kwa mwaka, au mara moja, yanakadiriwa kuwa karibu $443m baada ya kutozwa ushuru.
Mwenyekiti wa kampuni ya Powerball Charlie McIntyre amesema kupitia taarifa kwamba kuna tiketi nyingine sita - zilizouzwa Connecticut, Illinois, Louisiana, New Mexico, Pennsylvania na visiwa vya Virgin Islands - ambapo kila mmoja alishinda $2m.
Tiketi nyingine zilishinda $1m.
Maafisa wa mashindano ya bahati nasibu Massachusetts awali walisema tiketi hiyo iliuzwa Watertown, Boston lakini baadaye wakasahihisha hilo Alhamisi asubuhi.
Haijabainika kosa hilo lilitokea vipi.
Uwezekano wa kushinda jackpot hiyo ulikuwa moja kati ya 292.2 milioni

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...