Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Jumanne 22.08.2017

MTEULE THE BEST


Kylian MbappeHaki miliki ya pichaGOOGLE
Image captionKylian Mbappe
Paris Saint- Germain wanakaribia kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, na Fabinho kwa pauni milioni 200. Mbappe pekee atagharimu pauni milioni 128. PSG pia watamtoa na Lucas Moura katika mkataba huo. (Sky Sport)
Barcelona wamekubali kuwa Liverpool hawatowauzia Philippe Coutinho, 25, mwezi huu. (Mirror)
Kiungo wa Real Madrid Mateo Kovacic, 23, amekubali kwa kauli kujiunga na Liverpool kuziba nafasi ya Philippe Coutinho iwapo ataondoka kwenda Barcelona. (Daily Mirror)
Liverpool bado wanataka kumsajili Virgil van Dijk na watakuwa tayari ikiwa Southampton watabadili msimamo wao kuhusu beki huyo. (Liverpool Echo)
Diego CostaHaki miliki ya pichaEPA
Image captionDiego Costa
Diego Costa, 28, ameambiwa na Atletico Madrid atafute suluhu na Chelsea kwanza kabla ya kununuliwa kwa pauni milioni 25. (Sun)
Kiungo wa Juventus Claudio Marchisio anataka kuondoka Italia na kujiunga na Chelsea. (Corriere della Sera)
Manchester City wanakaribia kukata tamaa ya kumsajili beki wa West Brom Jonny Evans, 29, na badala yake watapanda dau la pauni milioni 20 kumtaka beki wa Middlesbrough Ben Gibson, 24. (Independent)
Ross Barkley
Image captionRoss Barkley
Tottenham wanajiandaa kupanda dau la pauni milioni 20 kumtaka kiungo wa Everton Ross Barkley, 23, ingawa wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Chelsea pia. (Telegraph)
West Ham tayari wanatafuta kocha wa kuziba nafasi ya Slaven Bilic ambaye amekuwa na mwanzo mbovu wa msimu. (Mirror)
Manchester United wanamtaka kinda wa Fulham Ryan Ssesegnon, 17, ambaye pia anasakwa na Tottenham. (Sky Sports)
Valencia wanakaribia kukamilisha usajili wa mkopo wa kiungo wa Manchester United Andreas Pereira. (Cadena Ser Valencia)
Julian Draxler
Image captionJulian Draxler
Bayern Munich wanafikiria kumsajili mshambuliaji wa Paris Saint-Germain Julian Draxler ambaye hatma yake iko mashakani baada ya kuwasili kwa Neymar. Draxler pia ananyatiwa na Arsenal, Liverpool na Manchester United. (Westdeutsche Allgemeine Zeitung)
Meneja wa Leicester Craig Shakespeare amesema hatma ya Riyad Mahrez, 26, na Danny Drinkwater, 27, pengine haitafahamika mpaka siku za mwisho za dirisha la usajili. (Leicester Mercury)
Beki wa kati wa Southampton ameonekana akifanya mazoezi na kikosi cha chini ya miaka 23 baada ya kuwasilisha maombi ya kuondoka. (Express)
Chelsea hawatopanda dau la kumtaka Virgil van Dijk hadi pale Southampton watakapokuwa tayari ingawa klabu hiyo imesema beki huyo hauzwi. (Telegraph)
Chelsea huenda wakaweza kumsajili Antonio Candreva, 30, kwa sababu Inter Milan inatafuta fedha za kutaka kumsajili Suso, 23, kutoka AC Milan. (Gazzetta dello Sport)
Kierran GibbsHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKierran Gibbs
Galatasaray wanataka kumsajili beki wa Arsenal Kieran Gibbs. (The Times)
Crystal Palace wamepanda dau la pauni milioni 15 kumtaka beki wa Tottenham Kevin Wimmer, ambaye pia anasakwa na West Brom na Stoke. Spurs wanataka pauni milioni 20. (Daily Mail)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...