Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mwanamume mchina alipia sahani 5000 za chakula baada ya kupata pete ya mpenzi wake iliyopotea

MTEULE THE BEST

TENCENT NEWS
Image captionWatu wapanga mlolongo kupata chakula
Mwanamume mmoja nchini China alilipia sahani 5000 za chakula kwenye mji ulio kusini magharibi mwa nchi wa Chongqing, baada ya pete aliyokuwa ampe mpezi wake na iliyokuwa imepotea kupatikana.
Kulingana na gazeti Chongqing Morning Post, mwanamume huyo kwa jina Wang, alikuwa na nia ya kumshangaza mpenzi wake kwa kumuomba akubali kumuoa, baada ya kuchumbiana kwa mwaka mmoja.
Alikuwa amefanya maandalizi ya mpango huo lakini wakati alipokuwa akipata chakula cha mchana, ghafla aliondoka kwenye kiti chake kwenda kupokea simu.
Aliporudi alipata kuwa mkoba wake uliokuwa na pete ya almasi yenye thamani ya dola 44,900 ulikuwa umetoweka.
Lakini kwa bahati nzuri mfanyakazi mmoja wa mkahawa aliupata mkoba huo na kuukabidhi kwa meneja Yue Xiaohua ambaye baadaye aliurejesha kwa Bwana Wang
Bwana Yue aliambia gazeti la Chingqing Morning Post, kuwa bwana Wang alirudi kwenye mkahawa huo siku iliyofuata na kuuliza kuwa ni sahani ngapi za chakula walikuwa wanauza kwa siku.
Kisha akalipa jumla ya dola 5,200 sawa na sahani 5000 za chakula akisema kila mtu aalikwe ili apate chakula.
Gazeti hilo pia lilisema kuwa bwana Wang aliandika barua ya kushukuru mkahawa huo akisema kuwa mpenzi wake aliikubali pete hiyo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...