Mwanamume mchina alipia sahani 5000 za chakula baada ya kupata pete ya mpenzi wake iliyopotea
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST
TENCENT NEWSImage captionWatu wapanga mlolongo kupata chakula
Mwanamume mmoja nchini China alilipia sahani 5000 za chakula kwenye mji ulio kusini magharibi mwa nchi wa Chongqing, baada ya pete aliyokuwa ampe mpezi wake na iliyokuwa imepotea kupatikana.
Kulingana na gazeti Chongqing Morning Post, mwanamume huyo kwa jina Wang, alikuwa na nia ya kumshangaza mpenzi wake kwa kumuomba akubali kumuoa, baada ya kuchumbiana kwa mwaka mmoja.
Alikuwa amefanya maandalizi ya mpango huo lakini wakati alipokuwa akipata chakula cha mchana, ghafla aliondoka kwenye kiti chake kwenda kupokea simu.
Aliporudi alipata kuwa mkoba wake uliokuwa na pete ya almasi yenye thamani ya dola 44,900 ulikuwa umetoweka.
Lakini kwa bahati nzuri mfanyakazi mmoja wa mkahawa aliupata mkoba huo na kuukabidhi kwa meneja Yue Xiaohua ambaye baadaye aliurejesha kwa Bwana Wang
Bwana Yue aliambia gazeti la Chingqing Morning Post, kuwa bwana Wang alirudi kwenye mkahawa huo siku iliyofuata na kuuliza kuwa ni sahani ngapi za chakula walikuwa wanauza kwa siku.
Kisha akalipa jumla ya dola 5,200 sawa na sahani 5000 za chakula akisema kila mtu aalikwe ili apate chakula.
Gazeti hilo pia lilisema kuwa bwana Wang aliandika barua ya kushukuru mkahawa huo akisema kuwa mpenzi wake aliikubali pete hiyo
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni