04/9/2017 Lil Wayne alazwa hospitalini kwa kuugua kifafa
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST
Image captionMwanamuziki wa nyimbo za kufoka Lil Wayne
Mwanamuziki Lil Wayne amekimbizwa hospitalini baada ya kuanguka kutokana na kifafa na kupatikana akiwa hana fahamu katika chumba cha hoteli alimokuwa huko Chicago.
Mtandao wa wasanii wa TMZ umesema mwanamuziki huyo wa nyimbo za kufoka, 34, anayeugua ugonjwa wa kifafa, ameangushwa na ugonjwa huo mara kadhaa na alipoteza fahamu pindi tu alipowasili huko A&E.
Alitarajiwa kuwatumbuiza mashabiki wake huko Las Vegas siku ya Jumapili usiku.
Nyota huyo, ambaye kwa jina lake rasmi Dwayne Michael Carter Jr, alipokea matibabu mwaka uliopita baada ya kupoteza fahamu mara mbili lakini kwa kiasi kidogo.
Miaka minne iliyopita Lil Wayne alikuwa akipokea matibabu kwa siku kadhaa katika hospitali moja huko Los Angeles.
Baada ya kupata fahamu, mwanamuziki huyo aliambia kituo cha redio cha Power 106 kwamba, anaugua ugonjwa wa kifafa na yuko katika hatari za kukosa fahamu mara kadhaa.
Alimwambia DJ Felli Fel: ''Hiyo haikuwa mara yake ya kwanza, pili, tatu, nne , tano, sita au saba … nimepatwa na kifafa mara kadhaa, ni vile huwa hampati habari hizo.''
Lil Wayne amesema hupoteza fahamu baada ya kupatwa na msongo wa kiakili, kutopumzika na kufanya kazi kupita kiasi.
Mashabiki waliokuwa na wasiwasi wamekuwa wakituma ujumbe kwenye mtandao wa Twitter kupitia #prayforweezy baada ya kisa cha mwanamuziki huyo kuripotiwa.
Mzaliwa huyo wa New Orleans, alianza taaluma hiyo akiwa na umri wa miaka 9, alipokuwa msanii mdogo kusajiliwa na rekodi ya Cash Money.
Tuzo zake tano bora za Grammy zinajumuisha tuzo ya albamu bora ya nyimbo za rap mwaka 2008 kwa albamu yake ya Tha Carter III na utumbuizaji bora wa rap kwa wimbo wake wa No Problem akiwa na Chance the Rapper & 2 Chainz
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni