Haki miliki ya pichaKCNAImage captionMarekani yataka kutwaliwa mali ya Kim Jong-un
Marekani imendekeza vikwazo vipya vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Korea Kaskazini, ikiwemo marufuku kwa biashara ya mafuta na kutwaliwa kwa mali ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.
Azimio lililowasilishwa kwa wanachama wa baraza la ulinzi wa Umoja wa Mataifa, linakuja baada ya jaribio la sita la nyuklia kufanywa na Korea Kaskazini.
Korea Kaskazini inadai kuunda bomu la haidrojeni na imekwua ikitishia kuishambulia Marekani.
China na Urusi zote zinatarajiwa kupinga vikwazo zaidi.
Korea Kaskazini tayari iko chini cha vikwazo vya kuitenga vilivyotangazwa na Umoja wa Mataifa, ambavyo vina nia ya kuulazimisha utawala wa nchi hiyo kusitisha mipango yake ya nyuklia.
Mwezi Agosti vikwazo vipya vya Umoja wa Mataifa vilipiga marufuku kuuzwa kwa mkaa wa mawe kutoka Korea Kaskazini ya thamani ya dola bilioni 1.
Haki miliki ya pichaKCNAImage captionPicha hii inadaiwa kuonyesha sherehe za jaribio la nyuklia la hivi majuzi
Pendekezo hilo la Umoja wa Mataifa linataka kuwekwa marufuku kabisa ya kuuzwa kwa bidhaa za mafuta kwenda Korea Kaskazini.
Pia pendekezo hilo linataka kutwaliwa kwa mali ya Bwa Kim na serikali ya Korea Kaskazini na pia kimpiga marufuku Kim mwenyewe na maafisa wengine wa vyeo vya juu kusafiri.
Wafanyakazi wa Korea Kaskazini nao watapiwa marufuku ya kufanya kazi nchi za kigeni.
Pesa zinazotumwa nyumbani kutoka nchi za kigeni na mauzo ya bidhaa za nguo ndizo peke zilizobaki kuiletea fedha Korea Kaskazini
Lakini Marekani inatarajiwa kukabiliana upinzani kutoka China na Urusi ambazo zote huuza mafuta kwa Korea Kaskazini na zina kura ya turufu katika Umoja wa Mataifa
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.
Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...
Maoni