Chama cha Kenyatta chapinga maafisa wapya wa uchaguzi Kenya
MTEULE THE BEST
Haki miliki ya pichaUHURU KENYATTA/TWITTERImage captionBw Kenyatta na naibu wake William Ruto
Chama cha Jubilee, chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, kimepinga kundi la maafisa tisa wakuu wa Tume ya Uchaguzi nchini humo ambao wanatarajiwa kusimamia uchaguzi mpya mwezi ujao.
Chama hicho kimetoa orodha ya majina ya maafisa hao ambao kinasema wanajulikana kwamba "wanapendelea upande fulani".
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi IEBC alitangaza kundi la maafisa saba watakaoongoza maandalizi ya uchaguzi utakaofanyika tarehe 17 Oktoba siku ya Jumanne.
Maafisa hao ambao wanajumuisha mkuu wa kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) na msimamizi wa kituo cha taifa cha kujumlishia matokeo watahudumu kwa miezi mitatu.
Mahakama ya Juu, ikifutilia mbali matokeo ya uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti ambapo Rais Kenyatta alitangazwa mshindi, iliiwekea lawama IEBC na kusema haikuandaa uchaguzi huo kwa njia na kwa kiwango kinachokubalika kikatiba.
Chama cha Jubilee kimesema: "Tuna habari za kuaminika kwamba kwenye orodha ya maafisa hao (watakaosimamia uchaguzi) kuna watu wanaofahamika wazi kuegemea upande Fulani."
"Ikizingatiwa makossa mengi ya kutotenda au ya kutenda ambayo yalichangia uchaguzi kufutiliwa mbali ambayo chanzo chake kilikuwa wafanyakazi wa IEBC, tunawasilisha pingamizi zetu kwa watu hawa tuliowataja hapa juu."
Muungano wa National Super Alliance (Nasa), ambao mgombea wake alikuwa waziri mkuu wa zamani Raila Odinga, ulikuwa umeitisha mabadiliko makubwa kwenye IEBC kabla ya uchaguzi mpya kufanyika.
Chama hicho kilisema hakitashiriki uchaguzi huo mpya iwapo mabadiliko hayatafanywa tume hiyo.
Haijabainika iwapo Bw Odinga na muungano wake wanakubaliana na majina ya watu walioteuliwa na Bw Chebukati.
Nasa hata hivyo wamepinga tarehe mpya iliyotangazwa na tume hiyo ya 17 Oktoba. Muungano huo umesema maafisa wa tume hawakushauriana nao kabla ya kutangaza tarehe hiyo.
Rais Kenyatta hata hivyo ameunga mkono tarehe hiyo na kusema hakuna hitaji la tume hiyo kushauriana na wanasiasa kabla ya kutangaza tarehe ya uchaguzi.
Bw Kenyatta, aliyekutana na viongozi wa kidini ikulu leo, amesema tarehe iliyotangazwa inafaa ili kutovuruga kalenda ya mitihani ya taifa ambayo imepangiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Oktoba.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.
Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...
Maoni