Chama cha Kenyatta chapinga maafisa wapya wa uchaguzi Kenya
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST
Haki miliki ya pichaUHURU KENYATTA/TWITTERImage captionBw Kenyatta na naibu wake William Ruto
Chama cha Jubilee, chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, kimepinga kundi la maafisa tisa wakuu wa Tume ya Uchaguzi nchini humo ambao wanatarajiwa kusimamia uchaguzi mpya mwezi ujao.
Chama hicho kimetoa orodha ya majina ya maafisa hao ambao kinasema wanajulikana kwamba "wanapendelea upande fulani".
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi IEBC alitangaza kundi la maafisa saba watakaoongoza maandalizi ya uchaguzi utakaofanyika tarehe 17 Oktoba siku ya Jumanne.
Maafisa hao ambao wanajumuisha mkuu wa kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) na msimamizi wa kituo cha taifa cha kujumlishia matokeo watahudumu kwa miezi mitatu.
Mahakama ya Juu, ikifutilia mbali matokeo ya uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti ambapo Rais Kenyatta alitangazwa mshindi, iliiwekea lawama IEBC na kusema haikuandaa uchaguzi huo kwa njia na kwa kiwango kinachokubalika kikatiba.
Chama cha Jubilee kimesema: "Tuna habari za kuaminika kwamba kwenye orodha ya maafisa hao (watakaosimamia uchaguzi) kuna watu wanaofahamika wazi kuegemea upande Fulani."
"Ikizingatiwa makossa mengi ya kutotenda au ya kutenda ambayo yalichangia uchaguzi kufutiliwa mbali ambayo chanzo chake kilikuwa wafanyakazi wa IEBC, tunawasilisha pingamizi zetu kwa watu hawa tuliowataja hapa juu."
Muungano wa National Super Alliance (Nasa), ambao mgombea wake alikuwa waziri mkuu wa zamani Raila Odinga, ulikuwa umeitisha mabadiliko makubwa kwenye IEBC kabla ya uchaguzi mpya kufanyika.
Chama hicho kilisema hakitashiriki uchaguzi huo mpya iwapo mabadiliko hayatafanywa tume hiyo.
Haijabainika iwapo Bw Odinga na muungano wake wanakubaliana na majina ya watu walioteuliwa na Bw Chebukati.
Nasa hata hivyo wamepinga tarehe mpya iliyotangazwa na tume hiyo ya 17 Oktoba. Muungano huo umesema maafisa wa tume hawakushauriana nao kabla ya kutangaza tarehe hiyo.
Rais Kenyatta hata hivyo ameunga mkono tarehe hiyo na kusema hakuna hitaji la tume hiyo kushauriana na wanasiasa kabla ya kutangaza tarehe ya uchaguzi.
Bw Kenyatta, aliyekutana na viongozi wa kidini ikulu leo, amesema tarehe iliyotangazwa inafaa ili kutovuruga kalenda ya mitihani ya taifa ambayo imepangiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Oktoba.
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni