Bomu la Korea Kaskazini lilisababisha 'maporomoko ya ardhi'
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
-
MTEULE THE BEST
Haki miliki ya pichaPLANET / 38 NORTHImage captionPicha za 38 North zinaonesha maporomoko kadha yaliyokea karibu na kilele cha Mlima Mantap
Majaribio ya bomu la nyuklia ambayo yalifanywa na Korea Kaskazini Jumapili yalisababisha maporomoko kadha ya ardhi, kwa mujibu wa picha za setilaiti ambazo zinaaminika kuwa za kwanza kabisa za eneo ambalo majaribio hayo yalifanyika.
Majaribio hayo ya bomu yalifanyika chini ya ardhi katika eneo la kufanyia majaribio silaha linalotumiwa na Korea Kaskazini la Punggye-ri ambalo lina milima mingi.
Kundi la uchunguzi kwa jina 38 North limechapisha picha ambazo zinaonekana kuonyesha "maporomoko kadha katika eneo kubwa" kuliko yaliyowahi kushuhudiwa awali.
Mlipuko wa bomu hilo ulisababisha tetemeko la ardhi la nguvu ya 6.3 kwenye vipimo vya Richter.
Tetemeko hilo lilisikika hadi China na katika baadhi ya maeneo ya Urusi.
Korea Kaskazini imefanya majaribio sita ya silaha za nyuklia kufikia sasa, yote katika eneo la Punggye-ri, ambalo lina njia za chini kwa chini ambazo zimechimbwa ndani kwenye milima.
Picha za karibuni zaidi za 38 North zilipigwa siku moja baada ya majaribio hayo kufanywa na zinaonesha maporomoko pamoja na maeneo yenye vifusi na matope.
Kuna pia maeneo ya ardhi ambayo inaonekana yalirushwa juu angani lakini yakarejea tena chini bila kuhama.
Haki miliki ya pichaPLANET / 38 NORTHImage captionPicha ya karibu katika eneo la majaribio ya silaha ya Punggye-ri iliyopigwa siku chache kabla ya jaribio la Jumapili...Haki miliki ya pichaPLANET / 38 NORTHImage caption...ukilinganisha na picha ya eneo hilo iliyopigwa Jumatatu.
Uharibifu ulitokea karibu na Mlima Mantap, mlima mrefu zaidi eneo hilo la majaribio.
Waliochunguza eneo hilo wamesema kulikuwa na "maporomoko makubwa na yaliyoenea sana kuliko tuliyoshuhudia wakati wa majaribio matano ya awali ambayo Korea Kaskazini iliyafanya."
Lakini waliongeza kwamba ingawa tetemeko hilo lilisababisha tetemeko lenye nguvu sana, hakuna dalili kwamba njia ya chini kwa chini ambayo ilitumiwa kulipua bomu hilo iliporomoka.
Baadhi ya wataalamu wanaamini kwamba mlipuko wa bomu ulisababisha shimo ambalo lilitumiwa kulipua bomu hilo Punggye-ri liliporomoka, sana kutokana na hali kwamba kulitokea tetemeko la pili mwendo wa dakika nane baada ya tetemeko la kwanza.
Haki miliki ya pichaPLANET / 38 NORTHImage captionPicha ya Punggye-ri kabla ya majaribio inaonesha eneo hilo lilikuwa na miti, nyasi na majani...Haki miliki ya pichaPLANET / 38 NORTHImage captionLakini picha ya baada ya majaribio inaonesha maeneo ya milima hiyo yakiwa wazi, dalili kwamba kulitokea maporomoko ya ardhi
Bomu la Jumapili linakadiriwa kuwa na nguvu ya kati ya kilotani 50 na 120.
Bomu la nguvu ya kilotani 50 linakadiriwa kuwa na nguvu mara tatu ukilinganisha na bomu la nyuklia lililoangushwa na Marekani katika mji wa Hiroshima mwaka 1945.
Majaribio kufanywa eneo moja Korea Kaskazini yameibua wasiwasi kuhusu iwapo eneo hilo linaweza kuwa hatari, ingawa wataalamu wamegawanyika.
Mapema wiki hii, wanasayansi wa China walieleza wasiwasi kwamba mlima huo unaweza kuporomoka na kutoa miali nururishi iwapo majaribio yataendelea kufanywa eneo hilo, gazeti la South China Morning Post liliripoti.
Lakini shirika la 38 North awali lilikuwa limesema hakuna uwezekano wa majaribio hayo kusababisha mlipuko wa volkano katika milima hiyo.
Marekani inaweza kuishambulia Korea Kaskazini?
Mzozo huo umekuwa ukiendelea kwa miaka mingi, lakini hali kwamba Korea Kaskazini inakaribia kuwa na/ au tayari ina uwezo wa kuunda kichwa kidogo cha nyuklia kinachoweza kuwekwa kwenye makombora, na kwamba ina makombora yanayoweza kufikia Marekani bara, yanabadilisha mambo sana.
Miezi kadha iliyopita, kumekuwa na hatua za 'uchokozi' mara kadha za Korea Kaskazini pamoja na majibizano kati yake na Marekani ambazo zimezidisha mzozo huo.
Korea Kaskazini ilitishia kurusha mabomu karibu na kisiwa cha Guam ambacho kinamilikiwa na Marekani katika Bahari ya Pacific.
Majuzinchi hiyo imerusha kombora kupitia anga ya Japan.
Lakini huku majibizano yakiendelea, bado ni vigumu kubashiri ni nini kitafuata.
Image captionUwezo wa makombora ya Korea Kaskazini
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni