Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Austria kumchagua kiongozi mwenye umri mdogo zaidi duniani

MTEULE THE BEST
Austria kumchagua kiongozi mwenye umri mdogo zaidi duniani
Mkuu wa chama cha kihafidhina nchini Austria cha People's Party, Sebastian Kurz, anaelekea kuwa kiongozi wa taifa mwenye umri mdogo duniani, baada ya ushindi wake katika uchaguzi mkuu hapo jana.
Kurz aliye na umri wa miaka 31 amepungukiwa na uwingi , lakini yupo katika nafasi nzuri ya kuunda serikali ya muungano.
Kijana aponzwa na Adolf Hitler Austria
Haijulikani wazi iwapo atafikiria kuunda serikali ya muungano na chama kinachopinga uhamiaji Freedom Party, kilichoibuka nafasi ya tatu kwa kishindo katika uchaguzi huo.
Akihutubia wafuasi wake Bw Kurz alisema: "Ni wakati wa kuleta mabadiliko kati nchi hii. Leo ni siku muhimu kwetu kuibadilisha nchi hii na ninasema asante kwa wale wamewezesha hili".
"Nina furaha, nimejitolea kuifanyia kazi Austria."
Sebastian Kurz ni nani?
Kabla ya uchaguzi Bw. Kurz lihudumu kama waziri mwenye umri mdogo zaidi wa mashauri ya nchi za kigeni barani ulaya, baada ya kuteuliwa mwaka 2013 akiwa na umri wa miaka 27.
Mwezi Mei mwaka 2017 akawa kiongozi wa chama cha People's Party. Alianza taaluma yake ya siasa katika tawi la vijana wa chama kabla ya kwenda kuhudumu katika baraza la manispaa la mji wa Vienna.
Nyumba ya Adolf Hitler kuvunjwa Austria
Akipewa jina "Wunderwuzzi" linalomaanisha mtu anayeweza kutembea juu ya maji, amefananishwa na viongozi vijana wa Ufaransa na Canada, Emmanuel Macron na Justin Trudeau.
Sawa na Macron, Bw Kurz amejiundia wafuasi wanaomzunguka, kukibadilisha chama cha People's Party, ambacho kimekuwa madarakani kwa miak

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...