Hongera MAGUFULI: Barrick Gold kuilipa Tanzania dola milioni 300 za kimarekani sawa billion 700 za kitanzania
MTEULE THE BEST
Barrick Gold kuilipa Tanzania dola milioni 300 za kimarekani
Kampuni ya inayomiliki migodi ya madini nchini Tanzania, Barrick Gold imekubali kuilipa Serikali ya Tanzania hisa ya asilimia 16 na mgawo wa asilimia hamsini ya mapato ya mauzo ya dhahabu kutoka migodi 3 inayoimiliki.
Hatua hiyo ni utekelezaji wa sheria mpya za madini ya Tanzania baada ya kampuni hiyo kukubali kuwa na mazungumzo na Serikali ya Tanzania .
Vilevile kampuni hiyo imekubali kutoa Dola za Kimarekani milioni 300 kama malipo ya kuonesha nia njema ya kufidia fedha zilizotokana na upotevu wa mapato kutokana na biashara ya kampuni hiyo.
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo,Prof. Thornton amesema Barrick Gold Corporation watazingatia makubaliano haya na wanaamini kuwa yamefungua ukurasa muhimu utakaowezesha kufanya biashara kisasa.
Kampuni ya dhahabu kujadiliana na Tanzania kuhusu malipo
Tanzania yapoteza matrilioni ya pesa za madini
Mambo muhimu kuhusu sakata ya madini Tanzania
Kwa upande wake Rais wa Tanzania John Magufuli amesema makubaliano hayo yataisaidia nchi kuzalishaji ajira zaidi, kupata manufaa mbalimbali yanayostahili ikiwemo fedha za kugharamia huduma za kijamii kwa wananchi na yanajenga msingi imara ambao utaiwezesha Tanzania kunufaika na rasilimali zake za madini.
Wakati huohuo waziri wa Katiba na Sheria nchini humo Prof.Palamagamba Kabudi ambaye alikuwa kiongozi wa mjadala huo amesema sheria hiyo iliyopita mwezi july imeleta dira mpya katika biashara hiyo ya madini.
Barrick Gold kuilipa Tanzania dola milioni 300 za kimarekani
Kampuni ya inayomiliki migodi ya madini nchini Tanzania, Barrick Gold imekubali kuilipa Serikali ya Tanzania hisa ya asilimia 16 na mgawo wa asilimia hamsini ya mapato ya mauzo ya dhahabu kutoka migodi 3 inayoimiliki.
Hatua hiyo ni utekelezaji wa sheria mpya za madini ya Tanzania baada ya kampuni hiyo kukubali kuwa na mazungumzo na Serikali ya Tanzania .
Vilevile kampuni hiyo imekubali kutoa Dola za Kimarekani milioni 300 kama malipo ya kuonesha nia njema ya kufidia fedha zilizotokana na upotevu wa mapato kutokana na biashara ya kampuni hiyo.
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo,Prof. Thornton amesema Barrick Gold Corporation watazingatia makubaliano haya na wanaamini kuwa yamefungua ukurasa muhimu utakaowezesha kufanya biashara kisasa.
Kampuni ya dhahabu kujadiliana na Tanzania kuhusu malipo
Tanzania yapoteza matrilioni ya pesa za madini
Mambo muhimu kuhusu sakata ya madini Tanzania
Kwa upande wake Rais wa Tanzania John Magufuli amesema makubaliano hayo yataisaidia nchi kuzalishaji ajira zaidi, kupata manufaa mbalimbali yanayostahili ikiwemo fedha za kugharamia huduma za kijamii kwa wananchi na yanajenga msingi imara ambao utaiwezesha Tanzania kunufaika na rasilimali zake za madini.
Wakati huohuo waziri wa Katiba na Sheria nchini humo Prof.Palamagamba Kabudi ambaye alikuwa kiongozi wa mjadala huo amesema sheria hiyo iliyopita mwezi july imeleta dira mpya katika biashara hiyo ya madini.
Maoni