Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Serikali imesema itaanzisha madawati ya jinsia katika shule za msingi na sekondari





Serikali imesema itaanzisha madawati ya jinsia katika shule za msingi na sekondari, ili wanafunzi waripoti matukio ya kikatili wanayofanyiwa na wazazi na jamii inayowazunguka. 

Lengo la hatua hiyo ni kuendelea kupunguza vitendo hivyo vinayoendelea kushamiri nchini. 

Mkakati huo, ulitangazwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile, wakati akifungua mdahalo wa wahariri wa vyombo vya habari kuhusu ukeketaji, ndoa na mimba za utotoni katika kuelekea Siku ya Mtoto wa Kike Oktoba 11, jana jijini Dar es Salaam. 

Dk. Ndugulile alisema sababu ya kuanzisha madawati hayo katika shule ni baada ya kubaini wanaofanya vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa watoto chini ya miaka 18 ni wazazi, walezi, ndugu wa karibu na majirani. 

ā€œMatukio ya ukatili wa kijinsia yanaendelea kushamiri ndani ya jamii kwa sababu wanaohusika wapo ndani ya familia. Hivyo hayaripotiwi kwenye vyombo vya sheria na badala yake familia zinamalizana nyumbani tu kwa kupeana vitu kama ng'ombe, fedha na mali nyingine,ā€ alisema na kuongeza: 

ā€œSerikali sasa kwa kushirikiana na maofisa elimu, tumeanzisha madawati ya jinsia kwenye shule ili wanafunzi waweze kuripoti matukio haya wanayofanyiwa kwa walimu wao ambao watakuwa wamepewa mafunzo maalum." 

Pia serikali itaboresha madawati ya jinsia zaidi ya 500 yaliyopo katika vituo vya polisi nchini, ili matukio ya kikatili ya kijinsia kwa watoto yanayoripotiwa yapewe kipaumbele ili hatua za kisheria zichukuliwe haraka. 

Dk. Ndugulile alisema kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike inayoadhimishwa Oktoba 11 kila mwaka inasema ā€˜Imarisha uwezo wa mtoto wa kike; tokomeza ukeketaji, mimba na ndoa za utotoniā€™ ina lengo kuhamasisha jamii kushirikiana na serikali kumaliza matukio hayo ndani ya jamii. 

Alifafanua kauli mbiu hiyo inahamasisha jamii kushirikiana na serikali kupinga na kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto walio chini ya miaka 18. 

Alisema kwa mujibu wa takwimu za Ofisi ya Takwimu ya Taifa  (NBS), katika kipindi cha mwaka 2017 matukio 41,000 ya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto yaliripotiwa na kati ya hayo ya watoto peke yake yalikuwa 13,000. 

Alisema sababu za kuendelea kushamiri kwa matukio hayo ni mila na desturi potofu na umaskini unaochochea watoto wa kike kuolewa chini ya miaka 18. 

Alitaja madhara wanayopata ni ukatili wa kingono, mimba za utotoni, kukatisha ndoto zao na maambukizi ya magonjwa kama Ukimwi. 

Alisema mpango wa serikali ni kuhakikisha wanapunguza matukio hayo hadi kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2022. 

Dk. Ndugulile alisema njia watakazotumia kupunguza matukio hayo ni kukusanya takwimu, kuyasemea na kuyatolea taarifa matukio hayo yanayoripotiwa katika madawati ya jinsia. 

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa), Davis Lumala, alisema katika kuhakikisha wanakabiliana na changamoto za ukeketaji, mimba na ndoa za utotoni wamekuwa wakitoa elimu katika shule mbalimbali. 

Pia wameanzisha kampeni ya kupinga na kuzuia matukio ya ukatili wa kijinsia katika wilaya saba za Tanzania Bara na tatu za visiwani Zanzibar

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...