Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Fahamu mambo yanayochangia kupoteza hisia za mapenzi




Lipo jambo muhimu analopaswa kuzingatia kila aliye kwenye uhusiano ikiwa anataka kutosheka na penzi la mpenzi wake. 




Kwanza ni lazima uitosheleze akili yako, lakini pili, unapaswa kuamini kwamba uliyenaye ni bora na hata ikiwa kuna kasoro, jambo la msingi ni kuzungumza kuondoa tatizo hilo, siyo zaidi. 

Anachanganya mambo, hatosheki 
Ukweli ni kuwa wengi wa watu wanaodai hawatosheki katika mapenzi ni wale wanaoziachia akili zao zitake tendo la ndoa zaidi, bila kuangalia uwezo, nafasi, hisia na afya yao ya kukutana kimwili. 

Lakini pia wengine ni kwa sababu wanavuta hisia za wapenzi wao wa zamani, ambao labda walikuwa wana uwezo mkubwa zaidi katika tendo hilo kuliko sasa. 

Hata hivyo, wakati mwingine wanashindwa kuelewa kuwa hata wale wanaofikiri ni wazuri, kama wangekuwa nao hadi leo, huenda wasingeweza kuendelea kuwa imara. 

Hii ni kwa sababu, watu wengi baada ya kukaa pamoja kwa muda mrefu hupoteza nguvu au shauku ya tendo hilo. 

Zipo sababu nyingi za hali hiyo, mojawapo ni kutobadilika kwa mazingira au wapenzi kuanza kutoelewa kwa sababu mbalimbali kama vile kutojaliana na kadhalika. 

Nguvu za kijinsia 
Kama hukuwa unafahamu; ni kwamba, idadi ya wanaume wasiyo na uwezo wa kufanya vyema tendo la ndoa inazidi kuongezeka. Tafiti zinabainisha kuwa wastani wa ndoa nne kati ya 10 zenye umri wa miaka 3 na kuendelea zinakabiliwa na tatizo hilo. 

Pia wanaume sita kati ya 10 wanasumbuliwa na tatizo la nguvu za kiume, kwamba kama siyo kuwa na uwezo mdogo, basi hukosa kabisa nguvu za kuendelea. 

Wengine wanaweza kuanza, lakini hawawezi kuendelea au wengine hata kuanza ni shida. 

Ingawa tiba yake ni ndogo, hasa mchanganyiko wa vyakula kama nilivyowahi kueleza mara kadhaa.Idadi kubwa ya wanaume bado wanasumbuliwa na tatizo hili, hasa kwa sababu ya kutokuwa tayari kuchukua hatua hasa za kuzingatia ushauri. 

Ziko sababu nyingi za kukumbwa na hali hii, ikiwamo ulevi, kutofanya mazoezi, kujichua au utumiaji holela wa vyakula, hasa vyenye mafuta. Hata hivyo, kwa kuzingatia tiba sahihi ya vyakula bora, mtu anaweza kupona. 

Kwa mfano kuna baadhi ya vyakula vikichanganywa kwa ustadi kama pilipili, parachichi na kadhalika vinaweza kumfanya mtu kuondokana na tatizo hilo. 

Wapenzi wa siku nyingi 

Wengi wa watu walio kwenye ndoa za miaka mingi, wanafanya mapenzi kwa sababu tu wamepata nafasi ya kuwa pamoja, lakini siyo kwa sababu ya kuwa na hisia kali. 

Matokeo yake ni wanandoa wengi hupata msisimko mdogo katika tendo la ndoa wanapokuwa na wenzi wao. Hata hivyo, kwa kuzingatia utaalamu, wanaweza kuwa na furaha katika ndoa yao

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...