Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mbwana Samatta: Sababu ya mshambuliaji wa Tanzania kung’ang’aniwa na klabu za West Ham, Everton na Burnley Englan

Mbwana Samatta: Sababu ya mshambuliaji wa Tanzania kung’ang’aniwa na klabu za West Ham, Everton na Burnley England
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Ally Samatta anang'ang'aniwa na klabu tatu za England, taarifa za vyombo vya habari nchini Uingereza zinasema.
Tetesi zinasema nyota huyo anatafutwa na West Ham United, Everton na Burnley.
Samatta, 25, maarufu kwa Watanzania kama Samagoal ameng'aa sana akichezea klabu ya KRC Genk nchini Ubelgiji.
Amefungia klabu hiyo mabao 11 katika mechi 16 ambazo amewachezea msimu huu, nusu ya mabao hayo akiyafunga barani Ulaya.
Samatta asaidia klabu yake kufuzu Europa League
Utafiti: Mbwana Samatta, Salim Kikeke wana ushawishi mkubwa Tanzania
Kylian Mbappe ana uhusiano na Tanzania?
Jedwali la Msimamo wa ligi ya EPL 2018/19
Taarifa za kumhusisha Samatta na klabu ya Everton zimetoka kwa mtandao wa hitc.com, mmoja wa mitandao ambayo imeibukia kuwa maarufu kwa taarifa za wachezaji na kuhama kwao.
Kwa nini anahusishwa na Everton?
Samatta, mwenye kimo cha futi 5 inchi 11, amefunga mabao sita katika ligi ndogo ya klabu barani Ulaya, Europa League, na ni hapo ameanza kuonekana na klabu za England.
Mnamo 23 Agosti 2018 Samatta, alifunga 'hat-trick' dhidi ya Brøndby IF katika Europa League kwenye mechi ambayo walishinda 5-2.
Everton wametatizika kumpata mshambuliaji wa kutegemewa tangu nyota wao Romelu Lukaku alipowaacha na kuhamia Manchester United kwa £75 mwaka 2017.
Man Utd wakubali kumnunua Romelu Lukaku
''Lukaku aliondoka Everton kufuatia ujumbe wa uchawi''
Wachezaji wanaotumia lugha ya Lingala kuchanganya walinzi
Wamekumbwa na ukame wa mabao msimu huu na zaidi wamesaidiwa na mawinga au viungo wa kati badala ya washambuliaji wao ambao wameonekana butu.
Ndio maana si ajabu wanavutiwa na mchezaji ambaye ameibuka stadi wa kutikisa nyavu.
Walijaribu kujaza pengo kwa kumchukua mchezaji wao wa zamani Wayne Rooney lakini mshambuliaji huyo hakuvuma sana na mwishowe alihamia Marekani.
Mshambuliaji wao wa sasa Oumar Niasse, kwa mujibu wa msn.com anatarajiwa kuihama klabu hiyo ya Merseyside, na inaarifiwa meneja wao Marco Silva anatafuta mchezaji wa kujaza nafasi hiyo.
Cenk Tosun alikuwa amenunuliwa na klabu hiyo Januari lakini baada alianza vibaya kisha akaimarika kabla ya kudidimia tena. Mturuki huyo amewafungia bao moja pekee msimu huu. Alikuwa kwenye benchi mechi yao dhidi ya Leicester City Jumamosi.
Klabu nyingine za Ligi Kuu ya England - West Ham United, Burnley na Brighton - pia zinadaiwa kumfuatilia kwa karibu mchezaji huyo kutoka Afrika Mashariki.
Mchezaji wa asili ya Tanzania aliyecheza na kufunga Kombe la Dunia
Mkenya aliyecheza Kombe la Dunia Urusi
Mourinho hawezi kuficha hisia zake - Lukaku
Wayne Rooney aiongoza Everton kuilaza Gor Mahia Tanzania
Gazeti la Daily Mirror Jumamosi liliripoti kwamba West Ham wanamfuatilia mchezaji huyo ingawa walisema Everton wanaonekana kuwa na uzito zaidi wa kumtafuta ikizingatiwa kwamba Niasse anatarajiwa kuuzwa Januari.
Everton tayari wana uhusiano na Afrika Mashariki kupitia mdhamini wao SportPesa, na waliibuka kuwa klabu ya kwanza ya Ligi Kuu ya England kuchezea Afrika Mashariki walipocheza dhidi ya mabingwa wa ligi ya Kenya Gor Mahia katika Kombe la SportPesa Super Cup mwaka jana.
Watakuwa pia klabu ya kwanza ya England kuwa mwenyeji wa klabu ya soka ya Afrika Mashariki watakapowakaribisha nyumbani Gor Mahia uwanjani Goodison Park mwezi ujao.
Kuvuma akiwa TP Mazembe
Samatta alijiunga na Genk akitokea TP Mazembe Januari 2016 ambapo alitia saini mkataba wa kumuweka katika klabu hiyo hadi msimu wa 2019/20.
Amesalia na miezi 20 hivi kabla ya mkataba wake kumalizika.
Samatta alihamia Ubelgiji mwaka mmoja baada yake kutawazwa mchezaji bora wa mwaka Mwafrika aliyekuwa anacheza ligi za barani Afrika mwaka 2015.
Mataifa ya Afrika yanayowakilishwa na Ufaransa Kombe la Dunia
Wachezaji wa Everton watua Dar es Salaam
Alishinda vikombe sita vikuu akiwa na TP Mazembe ikiwa ni pamoja na kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mwaka 2015 kabla ya kuondoka.
Kufikia Machi mwaka huu, alikuwa ameichezea timu ya taifa ya tanzania mechi 44 na kuwafungia mabao 16 tangu alipowachezea mara ya kwanza mwaka 2011.
Samatta aliichezea Simba kabla ya kujiunga na TP Mazembe mnamo mwaka wa 2011.
Ingawa Mtanzania huyo amevuma sana msimu huu, ambapo alifunga mabao manane katika mechi 11 za kwanza, msimu uliopita hakufanya vyema sana. Alifunga mabao saba katika mashindano yote akichezea klabu yake msimu wa 2017/18.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...