Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Manchester United wamemshauri Zinedine Zidane 




Manchester United wamemshauri Zinedine Zidane kutotafuta umeneja kwingine wakati wakiamua hatma ya kocha wa sasa wa miamb hiyo ya England, Jose Mourinho. (Mirror) 

Mashabiki wa United walipigwa picha na bango la picha ya meneja wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zinade, 46 nje ya Old Trafford kabla ya ushindi wa siku ya Jumamosi dhidi ya Newcastle. (Eurosport) 

Machester United watahitajika kumlipa Mourinho pauni milioni 29 ikiwa watamfuta meneja huyo  lakini kiwango hicho kitashuka hadi paunia milioni 10 ikiwa atamaliza msimu na United washindwe kumaliza katika nafasi za Ligi ya Mabingwa. (Mirror) 

Mourinho alifichua kuwa alipokea ujumbe wa imani naye kutoka bodi ya Manchester United kabla ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Newcastle. (Times - subscription required) 

Tanguy Ndombele 
Manchester City watahitajika kuvunja rekodi yao ya kusaini wachezaji kwa kumsaini kiungo wa kati wa Lyon Tanguy Ndombele baada ya klabu hiyo ya ufaransa kumwekea thamani ya pauni milion 70 mchezaji huyo wa miaka 21 mwezi Januari. (Star) 

Manchester United wamemuambia Paul Pogba kuwa hatauzwa mwezi Januari licha ya mfaransa huyo kuripotiwa kuwa na nia ya kujiunga na Barcelona baada ya wao kuonyeha nia ya kumsaini. (Mail) 

Mousa Dembele 
Kiungo wa kati wa Tottenham Mousa Dembele, 31, hatarajiwi kujadili mkataba mpya na huenda akaondoka wakati mkataba wake utapokwisha msimu wa joto akitarajia kuhamia China au mashariki ya Kati. (Sun) 

Neymar 
Mshambuliaji nyota wa klabu ya Paris St-Germain na timu ya taifa ya Brazil Neymar amefanya mazungumzo na kiungo wa Manchester United Paul Pogba kumshawishi kujiunga na mabingwa hao wa League 1 baada ya kutokua na mustakabali mzuri wa baadae kwa kiungo huyu mwenye miaka 25. (Goal

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...