Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ijue Siri Ya Kuondokana Na Ukata




Siku ya leo katika pekua pekua zangu za kuongeza chakula cha ubongo nilikutana na kauli ambayo kiukweli ilifanya mishipa yangu ya ardenalini kuweza kushtuka kwa kasi kama vile nimeona kitu cha hatari sana. 

Kauli hiyo ilikuwa na maneno mawili yenye kubeba ujumbe mzito ambao sina uhakika kama, ujumbe huo upo mzani ambao ataweza kupima kilo zake, hii ni  kutokana na uzito uliopo katika ulipo katika ujumbe huo,  labda ujumbe huo upimwe na kichwa cha mwanadamu mwenye mtazamo chanya ndio anaweza kuuelewa. 

Ujumbe huo unasema ā€œunachokiogopa ndicho kitakachokuaā€ narudia kusema tena unachokiogopa ndicho kitakachokua. Kwa haraka haraka unaweza usielewe maana ya msemo huo ila pindi utulizapo fikra ya ujazo wa akili unaweza kuelewa. 

Binafsi nilichokielewa katika kauli hii ni kwamba, moja kati changamoto kubwa ambayo huwazuia watu wake kutoweza kutimiza makusudio yao hapa dunia ni kitu ambacho tunachokiita ni woga. 

Woga ndio ambao umekua tatizo sugu lilojengeka machoni mwa watu wengi hata kuwapelekea watu hao kuweza kufa maskini huku watu hao wana uwezo mkubwa wa kufanya mambo makubwa yenye kuleta mapinduzi ya kufikia kilele cha mafanikio yao. 

Woga huu si mwingine ni ule woga wa kuthubutu kuweza kufanya mambo mbalimbali. Wapo watu ambao wanatamani kufanya biashara kubwa ila wakiwatazama watu ambao walifanya biashara hiyo na kuona ya kwamba walifeli basi nao hujikuta wanaogopa kufanya jambo hilo. 

Achilia mbali biashara, wapo baadhi ya watu wanavipaji mbalimbali lakini watu hao wamekuwa ni waoga wa kuonesha vipaji hivyo machoni mwa watu wengine huku wakiamini ya kwamba watachekwa, watu wa aina hii mara nyingi hufa na ndoto zao. 

Wapo baaadhi ya watu wanaogopa kujenga nyumba zao za kuishi huku wakisema, ā€œkwa heshima niliyonayo nikijenga nyumba ya kawaida watu wengine wanatanishangaaā€ kwa kauli kama hizi basi hujikuta miaka inazidi kukatika bila watu hao kuweza kufanya kitu chochote cha maana. 

Wapo baadhi ya wanafanzi wamekuwa wanaogopa kusoma masomo ya sayansi huku wakiamini masomo hayo ni magumu mwisho wa siku watu hao hujikuta wanafeli masomo hayo, kwa mtazamo wa aina hii ndipo ninapokubaliana na kauli ile ambayo nimesema hapo awali ya kwamba unachokiogopa ndicho kitakachokua. 

Kabla sijamaliza kusema nawe siku ya leo nitakuwa ni mchoyo wa fadhira kama nitashindwa kutoa ufumbuzi wa tatizo hili, yawezekana ukawa na tatizo la aina hii ya kuogopa kufanya jambo fulani la maendeleo eti kwa sababu ya woga uliojengeke ndani mwako, unachotakiwa kukufanya ni kuhakakisha kila jambo ambalo unataka kulifanya, kabla hujaanza kulifanya jambo hilo hakikisha ya kwamba jambo hilo unalichunguza kwa makini  na sio kutanguliza woga mbele na ndiyo itakuwa siri ya kuondokana na ukata

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...