Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mambo 10 usiyofahamu kuhusu Hamisa Mobetto


Mrembo Hamisa Mobetto amejizolea umaarufu mkubwa kwenye kazi yake ya mitindo na urembo, hadi sasa kwenye muziki wa Bongo Fleva. Haya ni mambo 10 ya kawaida ambao huyafahamu kuhusu mrembo huyo. 

1. Sauti ya Hamisa Mobetto ndio inasikaka kwenye wimbo wa Diamond Platnumz, Lava Lava na Mbosso uitwao Jibebe.  Sauti ya mwanamke inayosikika 'I like ndio ya Hamisa. 

2. Kwa miaka miwili mfululizo Hamisa Mobetto ameshinda tuzo ya  Starqt Awards ambazo hutolewa nchini Afrika Kusini.Mwaka 2017 alishinda kupitia kipengele  cha People Choice Awards, pia aliwania kwenye kipengele cha Super Mum. Starqt Awards ni tuzo zinazohusisha biashara, mitindo, burudani na vitu vingine. 

3.Tangu akiwa mdogo Hamisa anakiri kuwa alipenda sana muziki na alitamani kuwa mwanamuziki. Kutokana na mahaba yake kwenye fedha akajikuta ameingia kwenye movie na mitindo. 

4. Mashabiki wengi wanajua kuwa wimbo wa kwanza Hamisa Mobetto kurekodi ni Madam Hero kutokana ndio wa kwanza kutoka kwake, hata hivyo Hamisa alianza kurekodi wimbo uitwao Furaha. 

5. Wimbo wa Hamisa, Madam Hero umeandikwa na msanii Foby na producer C 9. Utakumbuka Foby ndiye anahusika kwenye kuandika na kutunga  melody za wimbo wa Dayna Nyange na Bill Nass uitwao Komela. 

6. Mwaka 2010 Hamisa Mobetto alitwaa taji la Miss XXL, After School Bash. Mwaka 2011 alishiriki mashindano ya Miss Dar Indian Ocean na kushika nafasi ya pili, pia aliwahi kufanikiwa kuingia nusu fainali ya Miss Tanzania. 

7. Mashabiki wengi wanakumbukumbu ya Hamisa Mobetto kutokea kwenye video ya wimbo wa Diamond uitwao Salome. 

Kwa mujibu wa BBC Swahili video hiyo ndio iliongozwa kutazamwa zaidi nchini Kenya kwa mwaka 2016 ikiipita video, Work ya Rihanna na Drake. 

8. Kwenye wimbo wa Diamond Platnumz unaokwenda kwa jina la Nikifa Kesho, Hamisa Mobetto ndio amefanya back vocal za wimbo huo. 

9. Hamisa Mobetto ni Mrembo mwingine aliyewahi kushiriki mashindano ya Miss Tanzania na baada ya kutoshinda kuingia kwenye Muziki wa Bongo Fleva. 

Awali alifanya hivyo Jokate Mwegelo ambaye alikuwa mshindi namba mbili wa Miss Tanzania mwaka 2006, huyou ameweza kufanya kazi na wasanii wakubwa kama AY. 

10. Urafiki wa Hamisa Mobetto na Lira Garole ulianzia kwenye mtandao wa Instagram kwa kutumia Direct Message (DM). 

Kama ulikuwa hujui Lira Garole aliwahi kuwa mpenzi wa msanii Marekani, Chris Brown, pia alionekana kwenye video ya wimbo uitwao Sorry wa Rick Ross na Chris Brown

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...