Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Utafiti: Matumizi ya simu husababisha kuwa wapenzi wengi

Utafiti: Matumizi ya simu yaliyokithiri husababisha kuwa wapenzi wengi miongoni mwa wanafunzi



Matumizi ya simu yanasababisha wapenzi wengi?

Katika utafiti wa zaidi ya watu 3,400 nchini Marekani wanaosoma shahada ya kwanza, wale waliosema wana matatizo na muda wanaotumia katika simu zao wanaripotiwa kuwa na wapenzi wengi pia.


Na wanadhaniwa kuwa na msongo wa mawazo, mmoja wa watafiti amesema kuwa matokeo yautafiti yanashangaza.

Watafiti kutoka chuo kikuu cha Chicago, Cambridge na chuo kikuu cha Minnesota wamefanya tafiti hii ya tabia za uraibu wa simu.

Lengo la utafiti huu lilikua ni kutaka kujua hali ya afya ya akili ya wanafunzi na jinsi gani simu zina matokeo katika utendaji wao.

Ili kujua matumizi yaliyopitiliza ya simu za mkononi, wanafunzi waliulizwa maswali mbalimbali ikiwemo yafuatayo;

Rafiki zako na familia wanalalamika hukusu matumizi makubwa ya simu?


Una matatizo yoyote darasani kutokana na matumizi ya simu?


Unadhani muda unaotumia simu umeongezeka?


Tafiti imebaini uhusiano wa matatizo ya afya ya akili na utumiaji wa kupitiza wa simu

Mwanafunzi mmoja kati ya watano miongoni mwa waliojibu maswali walikubali maswali yote, na kuwafanya kuwa watumiaji wa kupitiliza wa simu, miongoni mwao wengi ni wanawake.

Kuacha mahusiano ya kawaida

Kwa hao wenye matumizi yaliyozidi ya simu za mkononi, wameripotiwa pia na uhusiano wa kimapenzi na zaidi ya mwenza mmoja katika kipindi cha miezi 12, kuliko wale waliokutwa hawana matumizi makubwa ya simu.

Alisilimia 37.7 ya wenye uraibu wa matumizi ya simu, wamekadiriwa kuwa na wapenzi hadi sita ndani ya miezi 12. Ikilinganishwa na asilimia 27.2 ya walioripotiwa kutokua na tatizo ya matumizi makubwa ya simu.

Dkt. Sam Chamberlain, mmoja kati ya waandishi wa tafiti hii kutoka chuo kikuu cha Cambridge anasema sababu ya suala hili ni ngumu kuijua.

''Inawezekana kuwa watu wanatumia sana simu na kukutana na wapenzi mtandaoni na wanaweza pia kusahau mahusiano ya kila siku kwa sababu ya matumizi yaliyokithiri ya simu za mkononi.''

"Kama hili suala lingekua na faida basi ingekua kinyume na matokeo badala yake afya ya akili ingekua imeimarika," ameongeza Dkt. Chamberlain.

Watafiti pia waligundua unywaji wa pombe kupita kiasi unawakumba wale wanaotumia simu kwa muda mrefu zaidi. Lakini hawakukutwa na uraibu mwingine wowote.

Baadhi ya wataalamu wamependekeza kuwa uchezaji wa 'game', ambao umewekwa katika kundi la tatizo na Shirika la Afya Duniani, ijumuishwe pia tatizo la kukaa muda mrefu katika vioo vya simu.

Tafiti za nyuma zimeonesha uhusiano wa kufeli kwa wanafunzi na matumizi ya simu, na ripoti hii pia ina uhusiano na suala hilo.

"Hata kama kuwa matokeo ya tatizo hili, yana madhara yake katika taaluma ya mtu na baadae katika kipindi chake cha kufanya kazi," amesema Profesa Jon Grant wa chuo kikuu cha Chicago.

Dkt Abigael San amesema kuwa anafurahia utafiti huu umefanyika: "haya madhara yote ni ya kweli na tunatakiwa kuyazingatia, watu wengi wanaweka tatizo hili kama tatizo la afya ya akili ama kuvunjika kwa mahusiano, lakini hayo yote yanachangiwa na matumizi ya simu za mkononi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...