Je wajua kuwa bingwa wa dunia wa
mbio za mita 800 za wanaume David rudisha ni afisa mkuu wa polisi nchini
Kenya? maelfu ya mashabiki wake walipigwa na butwaa alipochapisha picha
yake akiwa amevalia sare rasmi ya kikosi cha utumishi kwa wote katika
ukurasa wake wa mtandao wa Facebook.
Bingwa huyo na mshikilizi wa rekodi ya dunia ya mita 800 kwa upande wa wanaume ni afisa mkuu wa polisi
Picha hiyo inayomuonesha akiwa amevalia sare ya kikosi cha polisi inadhihirisha kuwa ni afisa wa ngazi ya juu.
Sio
aghalabu kuwa bingwa huyo na mshikilizi wa rekodi ya dunia ya mita 800
kwa upande wa wanaume ni afisa polisi, asilimia kubwa ya wanariadha
wakenya ni maafisa wa idara mbali mbali za vikosi vya ulinzi. Rudisha ametumika katika matangazo mengi tu ya kibiashara.
Hata hivyo hii ndio mara ya kwanza kwao kumuona Rudisha akiwa nadhifu na mtumishi kwa wote.
Wakenya wengi walisambaza picha hiyo katika mitandao ya kijamii.
kiongozi wa upinzani alidakia katika mjadala huo kwenye mitandao ya kijamii
Wengine walimuuliza iwapo 'Afande'' huyo pia
anapokea mlungula kama maafande wengine wa kitengo cha kuongoza magari
cha 'Trafiki' kama ilivyobainishwa katika uchunguzi wa maadili
unaoendelea nchini Kenya.
Hata hivyo Rudisha alichapisha ujumbe huo akiwarai mashabiki wake kote duniani wajivunie kazi zao.
\Rudisha alichapisha ujumbe huo akiwarai mashabiki wake kote duniani wajivunie kazi zao.
''Nafahamu kuwa wengi wenu mumezoea kuniona nikiwa
nimevalia jezi zangu za riadha , lakini hivi ndivyo ninavyovaa nikiwa
nje ya viwanja vya riadha ! Rudisha ni shabiki sugu wa Arsenal
Najivunia kuwa afisa wa polisi! #Loveyourjob''
Rudisha akijumuika na mwanawe katika zoezi
Rudisha amewahi kupata umaarufu mkubwa nchini kenya hususan alipovunja rekodi ya dunia ya mbio za mita 800.
Aidha ametumika katika matangazo mengi tu ya kibiashara.
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni