Je wajua kuwa bingwa wa dunia wa
mbio za mita 800 za wanaume David rudisha ni afisa mkuu wa polisi nchini
Kenya? maelfu ya mashabiki wake walipigwa na butwaa alipochapisha picha
yake akiwa amevalia sare rasmi ya kikosi cha utumishi kwa wote katika
ukurasa wake wa mtandao wa Facebook.
Bingwa huyo na mshikilizi wa rekodi ya dunia ya mita 800 kwa upande wa wanaume ni afisa mkuu wa polisi
Picha hiyo inayomuonesha akiwa amevalia sare ya kikosi cha polisi inadhihirisha kuwa ni afisa wa ngazi ya juu.
Sio
aghalabu kuwa bingwa huyo na mshikilizi wa rekodi ya dunia ya mita 800
kwa upande wa wanaume ni afisa polisi, asilimia kubwa ya wanariadha
wakenya ni maafisa wa idara mbali mbali za vikosi vya ulinzi. Rudisha ametumika katika matangazo mengi tu ya kibiashara.
Hata hivyo hii ndio mara ya kwanza kwao kumuona Rudisha akiwa nadhifu na mtumishi kwa wote.
Wakenya wengi walisambaza picha hiyo katika mitandao ya kijamii.
kiongozi wa upinzani alidakia katika mjadala huo kwenye mitandao ya kijamii
Wengine walimuuliza iwapo 'Afande'' huyo pia
anapokea mlungula kama maafande wengine wa kitengo cha kuongoza magari
cha 'Trafiki' kama ilivyobainishwa katika uchunguzi wa maadili
unaoendelea nchini Kenya.
Hata hivyo Rudisha alichapisha ujumbe huo akiwarai mashabiki wake kote duniani wajivunie kazi zao.
\Rudisha alichapisha ujumbe huo akiwarai mashabiki wake kote duniani wajivunie kazi zao.
''Nafahamu kuwa wengi wenu mumezoea kuniona nikiwa
nimevalia jezi zangu za riadha , lakini hivi ndivyo ninavyovaa nikiwa
nje ya viwanja vya riadha ! Rudisha ni shabiki sugu wa Arsenal
Najivunia kuwa afisa wa polisi! āŖ#āLoveyourjobā¬''
Rudisha akijumuika na mwanawe katika zoezi
Rudisha amewahi kupata umaarufu mkubwa nchini kenya hususan alipovunja rekodi ya dunia ya mbio za mita 800.
Aidha ametumika katika matangazo mengi tu ya kibiashara.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.
Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...
Maoni