Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wachezaji wa Everton watua Dar es Salaam Tanzania tayari kukabili Gor Ma

MTEULE THE BEST


Rooney na wachezaji wa Everton
Wachezaji wa klabu ya Everton kutoka England wamewasili jijini Dar es Salaam nchini Tanzania kwa ziara yao ya kwanza kabisa Afrika Mashariki.
Wachezaji hao na wakufunzi pamoja na maafisa wengine wa timu walifika uwanja wa ndege saa mbili asubuhi kutoka Liverpool.
Ziara yao ni sehemu ya maandalizi ya msimu ujao wa Ligi ya Premia.
Miongoni mwa wachezaji waliosafiri Tanzania ni Wayne Rooney ambaye amerejea katika klabu hiyo bila kulipiwa ada yoyote baada ya kukaa miaka 13 klabu ya Manchester United.
  • Wayne Rooney: Ninasubiri sana kwenda Tanzania
Wachezaji wa Everton
Mashabiki wengi wa soka ya England wamesafiri Tanzania kushuhudia Everton wakichuana na mabingwa wa Kenya, Gor Mahia katika uwanja wa taifa wa michezo jijini Dar es Salaam.
Uwanja huo una uwezo wa kutoshea mashabiki 60,000.
Rooney anatarajiwa kucheza katika mechi hiyo ya Alhamisi.
Wengi wa mashabiki waliofika nje ya hoteli wanamokaa Everton jijini Dar es Salaam waliimba "Rooney Rooney" mchezaji huyo aliposhuka kutoka kwenye basi kuingia hotelini.
Kulikuwa pia na kundi la raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambao walijawa na furaha kumuona mwenzao Yannick Bolasie.
Wachezaji wa Everton
Wachezaji ngoma wa Kimaasai waliofika kuwatumbuiza wachezaji hao
Image captionWachezaji ngoma wa Kimaasai waliofika kuwatumbuiza wachezaji hao
Wachezaji wa Everton
Waliimba nyimbo za kitamaduni za DR Congo naye Bolasie akawajibu kwa kucheza.
Mechi ya kesho imeandaliwa na kampuni ya SportPesa kusherehekea udhamini wa jezi za klabu ya Everton.
Wakati wa ziara yao, wachezaji wa Everton pia wataandaa vikao vya mafunzo ya soka na kucheza pia dhidi ya timu mseto ya wachezaji wenye matatizo ya ngozi, Albino United, kuhamasisha watu kuhusu mashambulio na dhuluma ambazo zimekuwa zikitendewa watu wenye ulemavu huo.
Wengi wamekuwa wakiuawa Tanzania na nchi jirani kwa sababu ya ushirikina.
Wachezaji hao baadaye wameelekea shule ya watoto wenye ulemavu ya Uhuru Mchanganyiko jijini Dar es Salaam.
Shule hiyo hupokea ufadhili kutoka kwa shirika la kutoa msaada nchi za nje la Uingereza, DFID.
Baadaye, wachezaji hao wanatarajiwa kucheza na watoto hao.
Wachezaji wa Everton wakiwa shule ya Uhuru Mchanganyiko
Image captionWachezaji wa Everton wakiwa shule ya Uhuru Mchanganyiko
Wachezaji wa Everton wakiwasalimia watoto
Image captionWachezaji wa Everton wakiwasalimia watoto
Kuwasalimia watoto
Mchezaji wa Everton akiwa amejifumba macho tayari kucheza na watoto
Image captionMchezaji wa Everton akiwa amejifumba macho tayari kucheza na watoto

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...