Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kiongozi mwingine akiapishwa litakuwa kosa la uhaini Kenya

MTEULE THE BEST


Mwanasheria mkuu wa Kenya Prof Githu Muigai amesema jaribio lolote la kumuapisha kiongozi mwingine wa Kenya litakuwa ni uhaini wa hali ya juu.
Prof Muigai amesema hayo huku kiongozi wa upinzani nchini humo Raila Odinga akisisitiza kwamba ataapishwa kuwa rais Jumanne wiki ijayo.
Bw Odinga alitangaza mwezi uliopita kwamba ataapishwa na Mabunge ya Wananchi ambayo yalipendekezwa na muungano wa upinzani National Super Alliance (Nasa).
Ingawa hakumtaja mtu yeyote, Prof Muigai, akiwahutubia wanahabari Nairobi, alisema shughuli hama hiyo ya kumuapisha kiongozi ambaye hajatangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC) haina msingi wowote kikatiba na kwamba itakuwa "bure na batili".
"Sheria za jinai za Jamhuri ya Kenya zinazungumzia shughuli kama hiyo kuwa uhaini wa hali ya juu," amesema.
"Wanaoshiriki watakuwa wanajihusisha katika uhaini wa hali ya juu, pamoja na wote wanaofanikisha shughuli kama hiyo."
Adhabu ya kosa la uhaini kwa mujibu wa sheria za Kenya ni kifo.
Prof Muigai amesema Mabunge ya Wananchi ambayo yanaundwa na Nasa pia ni kinyume cha sheria.
Bw Kenyatta aliapishwa kwa muhula wa pili tarehe 28 Novemba
Kufikia sasa, mabunge 12 ya majimbo, ikiwa ni pamoja na Mombasa, ambayo yanaongozwa na magavana wa muungano wa Nasa tayari yamepitisha azimio la kuundwa kwa mabunge hayo ya wananchi.
Kenya kwa jumla ina majimbo 47.
Nasa ilipendekeza kuundwa kwa mabunge hayo kama njia ya kushinikiza mageuzi nchini humo baada ya kususia uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 26 Oktoba.
Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi wa uchaguzi huo ambao ulisusiwa na upinzani.
Alipata kura 7.5 milioni, sawa na asilimia 98 ya kura zilizopigwa ingawa waliojitokeza walikuwa asilimia 39.
Bw Kenyatta aliapishwa kuwa rais tarehe 28 Novemba kwenye sherehe ambayo upinzani ulisusia.
Bw Odinga amesisitiza kwamba muungano wake hautambui ushindi wa Kenyatta na kwamba hautamtambua kama kiongozi halali wa nchi hiyo.
Marekani imemtaka Bw Odinga kuacha mpango huo wake wa kuapishwa kama rais wa nchi hiyo.
Waziri msaidizi wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika, Donald Yamamoto ambaye alikuwa amezuru Kenya alimtahadharisha Bw Odinga na pia akahimiza kuwepo mashauriano kati yake na serikali iliyopo madarakani.
Aidha alitahadharisha dhidi ya matendo ambayo yako nje ya katiba nchini humo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...