Raila Odinga
Marekani imemtaka kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga kuacha mpango wake wa kuapishwa kama rais wa nchi hiyo wiki ijayo.
Odinga aliwasilisha kesi juu ya mapungufu katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 8 Agosti katika Mahakama ya Juu nchini humo ambayo ilibatilisha uchaguzi huo na kuagiza uchaguzi wa marudio ufanyike.
Bw Odinga na muungano wake wa National Super Alliance hata hivyo walisusia uchaguzi huo wa 26 Oktoba ambapo Bw Kenyatta alitangazwa mshindi na mwishowe kuapishwa kwa muhula wa pili.
Waziri msaidizi wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika, Donald Yamamoto ambaye alikuwa amezuru Kenya alimtahadharisha Bw Odinga na pia akahimiza kuwepo mashauriano kati yake na serikali iliyopo madarakani.
Aidha alitahadharisha dhidi ya matendo ambayo yako nje ya katiba nchini humo.
Baadhi ya viongozi wa serikali wameonya kuwa tukio hilo la kuapishwa linaweza kuhusishwa na uhaini.
Mshauri wa Bw Odinga Salim Lone alipuuzilia mbali onyo hilo la Marekani na kusema Bw Odinga ataapishwa kama ilivyopangwa Jumanne wiki ijayo.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni