Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Iran yaonya iko tayari kurejesha mpango wake wa kinyuklia


Iran imeonya iko tayari kurejesha mpango wake wa kutengeza silaha za kinyuklia kwa kile ilichokitaja kasi kubwa zaidi iwapo Marekani itajiondoa kutoka makubaliano yaliyofikiwa mwaka 2015 kuhusu mpango huo wa kinyuklia.

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Javad Zarif ameonya kuwa iwapo Marekani itajiondoa kutoka makubaliano hayo yajulikanayo JCPOA, basi nchi yake haitakuwa na budi bali kuongeza kasi shughuli zao za kinyuklia.


Mapema mwezi huu, Rais wa Iran Hassan Rouhani alionya kuwa Marekani itajuta iwapo itajiondoa kutoka kwa makubaliano hayo yaliyofikiwa kati ya nchi sita zenye nguvu zaidi duniani na Iran yanayolenga kudhibiti mpango wa kinyuklia wa Iran na badala yake nchi hiyo ilegezewe vikwazo vya kiuchumi.

Je, Marekani itajiondoa kutoka JCPOA?

Rais wa Marekani Donald Trump amezitaka nchi za Ulaya kufanyia marekebisho makubaliano hayo ifikapo tarehe 12 mwezi Mei kwa kuiwekea Iran mbinyo zaidi la sivyo Marekani itajiondoa kutoka kwa makubaliano hayo yaliyofikiwa wakati wa utawala wa Barack Obama.

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Javad Zarif

Suala hilo kuhusu hatma ya makubaliano hayo ya JCPOA ya mwaka 2015, litakuwa mojawapo ya ajenda kuu wakati wa ziara ya Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron mjini Washington inayoanza Jumatatu na pia Kansela wa Ujerumani Angela Merkel mbaye pia ataizuru Marekani Ijumaa wiki ijayo kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Donald Trump.

Zarif amesema viongozi wa nchi za Ulaya wanapaswa kumshinikiza Trump kuheshimu makubaliano hayo iwapo Marekani inataraka kudumisha hadhi yake ya kuaminiwa katika jamii ya kimataifa.

Viongozi wa Ulaya wanatumai kumshawishi Trump kuyaokoa makubaliano hayo kuhusu Iran yaliyoko mashakani na kwa upande wao wataishinikiza Iran kufikia makubaliano kuhusu kusitisha majaribio ya makambora na kupunguza ushawishi wao katika nchi za kanda ya Mashariki ya Kati zinazokumbwa na mizozo- Yemen, Syria na Lebanon.

Iwapo Marekani itajiondoa katika makubaliano hayo kuhusu mpango wa kinyuklia wa Iran, inahofiwa kuwa Iran huenda isiyaheshimu makubaliano hayo yaliyofikiwa pia na Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani na Urusi.

Iran yatoa vitisho

Akizungumza na wanahabari mjini New York, Marekani anakohuduria mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu amani, waziri wa mambo ya nje wa Iran Javad Zarif amesema ni bayana kuwa ulimwengu hauwezi kuitarajia nchi yake kutekeleza na kuyaheshimu makubaliano hayo wakati upande mwingine umeyavunja.

Kiwanda cha kinyuklia cha Arak nchini Iran

Zarif ameongeza kuwa Iran haina nia ya kutengeza bomu la kinyuklia lakini nchi hiyo itajibu kujiondoa kwa Marekani katika makubaliano hayo ya kihistoria kwa kuanza tena kutengeza uranium, kiuongo muhimu katika utengezaji wa mabomu ya kinyuklia.

Iran imesema kuwa hatua ya Marekani kutaka kufanyia mageuzi vipengele vya makubaliano hayo unatuma ujumbe hatari sana kwa Wairan na ulimwengu kwa jumla kuwa nchi hazipaswi kufikia makubaliano na Marekani na pia kuwaonya Merkel na Macron kuwa kujaribu kumfurahisha Trump kuhusiana na suala hilo itakuwa na jaribio litakalofeli.

Trump anaamini kuwa makubaliano hayo ya JCPOA yana mapungufu makubwa ambayo yanahitaji kushughulikiwa ili kuizuia Iran kuwa na mwanya wa kuendeleza mpango wake wa kinyuklia

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...