Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mabadiliko baraza la mawaziri Tanzania: Magufuli amfuta kazi Mwigulu Nchemba, Zitto Kabwe na Pole Pole walumbana


Mwigulu Nchemba

Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amelifanyia mabadiliko baraza lake la mawaziri chini ya kipindi cha mwaka mmoja


Aliyeathirika na mabadiliko ya Rais Magufuli siku ya Jumapili ni waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Lameck Nchemba ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.


Mwigulu Nchemba alipata umaarufu kwa juhudi zake za kuzuia maandamano dhidi ya Rais Magufuli.


Alinukuliwa akitishia kuwalemaza waandamanaji na ''kuwakamata hata watakaoandamana wakiwa nyumbani".




Licha ya hapo awali kuhamishwa kutoka wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi, hadi wadhfa wake wa mwisho, Nchemba ameondolewa baada ya kuhudumu kwa miaka miwili katika baraza la Rais Magufuli.


Mbunge huyo wa Iramba aliyechukua nafasi ya aliyekuwa waziri Charles Kitwanga, sasa atampisha mbunge mwenzake kutoka Jimbo la Mwibara, Kangi Alphaxard Lugola kujaza pengo hilo.



Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @zittokabwe

Lugola amepandishwa wadhfa kutoka ofisi ya makamu wa rais muungano na mazingira ambapo alikuwa naibu waziri. Nafasi yake imechukuliwa na mbunge wa jimbo la Singida mjini Mussa Ramadhani Sima.


Katika mabadiliko mengine , Waziri Makame Mbarawa aliyesimamia wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano amebadilishana wadhifa na mwenzake wa wizara ya maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe.



Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @hpolepole

Vilevile wizara ya kilimo imeongezewa naibu waziri moja zaidi.


Mbunge wa Morogoro kusini mashariki Omary Tebwete Mgumba ameteuliwa kushirikiana na Dkt. Mary Mwanjelwa aliyekuwa naibu pekee kwenye Wizara hiyo.


Mkurugenzi wa jiji la Arusha Athumani Kihamia amehamia tume ya taifa ya uchaguzi NEC lakini amedumisha cheo chake kwani ameteuliwa kuwa mkurugenzi katika tume hiyo.




Athumani amepata mwanya baada ya aliyekuwa akishikilia wadhfa huo, Ramadhani Kailima kupandishwa ngazi hadi naibu katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi.



Rais Mgufuli na Mwigulu Nchemba

Ingawa waziri wake ameng'olewa, Balozi Hassan Simba Yahya, aliyekuwa naibu katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi, amepata nafuu kwa kupewa ubalozi huku Ikulu ikiahidi kufafanua kituo chake cha kazi hapo baadaye.


Uteuzi mwingine ni wa viongozi mbalimbali wa taasisi za idara tofauti za serikali.


Maafisa hawa wataapishwa siku ya Jumatatu katika Ikulu ya rais.


Mabadiliko haya yanajiri baada ya Rais Magufuli kuzidisha idadi ya wizara kwenye serikali yake kutoka 19 hadi 21 alipotenganisha wizara ya Nishati na Madini na kilimo na ile ya mifugo na uvuvi


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...