Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Redoine Faid: Jambazi sugu aliyetoroka jela kwa kutumia helikopta Ufaransa



Jambazi sugu ametoroka jela kwa kutumia ndege aina ya helikopta katika jela moja mjini Paris , mamlaka ya Paris imesema.


Redoine Faid alisaidiwa na watu kadhaa waliojihami ambao walitengeneza mwanya katika lango la jela hiyo huku helikopta hiyo ikitua katika uwanja karibu na jela hiyo.

Ndege hiyo ilipaa hadi eneo la Gonessa lililopo karibu na jela hiyo ambapo ilipatikana na maafisa wa polisi.

Faid 46, amekuwa akihudumia kifungo cha miaka 25 kwa jaribio la wizi wa mabavu lililotibuka ambapo afisa mmoja wa polisi aliuawa.



Hii ni mara yake ya pili kutoroka jela: Mwaka 2013 alitoroka jela baada ya kuwatumia walinzi wanne kama ngao huku akilipua milango kadhaa kwa kutumia kilipuzi.

Alifanikiwa kutoroka chini ya nusu saa baada ya kuwasili katika jela hiyo iliopo kaskazini mwa Ufaransa.

Mwaka 2009 Faid aliandika kitabu kuhusu uzoefu wake katika mitaa ya Paris iliojaa uhalifu na kuwa mtu aliyekukuwa akivunja sheria mara kwa mara.

Alidai kuwacha uhalifu lakini mwaka mmoja baadaye alihusika katika jaribio la wizi lililotibuka ambapo alipelekwa jela ya RĆ©au katika jimbo la Seine-et-Marne.

Faid na washirika wake walitorokea katika uwanja huo wa jela ambao haukuwa na ulinzi mkali, bila ya kumjeruhi yeyote kulingana na chombo cha habari cha Ufaransa Europe1.



Watu waliokuwa wamejihami kwa risasi walimchukua mfungwa huyo katika chumba cha kuwatembelea wageni kabla ya kumpeleka katika helikopta hiyo na kutoroka naye kulingana na duru za usalama zilizonukuliwa na chombo cha habari cha reuters.


Ripoti zinadai kwamba rubani wa helikopta huenda alikuwa ametekwa nyara. Usakaji wa maafisa wa polisi unaendelea katike eneo lote la Paris.

Hatua zote zinafanywa kumtafuta mtoro huyo , kulingana waziri wa maswala ya ndani.

Akiwa amezaliwa 1972, Faid alilelewa katika maeneo ya uhalifu mwingi ya mitaa ya Paris kabla ya kuanza maisha ya uhalifu



Miaka ya tisini , alikuwa akisimamia genge lililohusika na uhalifu wa kujihami na ulafi ktika mji mkuu wa Paris. Alikuwa akisema kwamba maisha yake yalipata msukumo wa filamu za uhalifu za Hollywood, ikiwemo Al Pacino na Scarface.

Mwaka 2001 alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa uhalifu

Maafisa wa polisi wa Ufaransa wanaamini kwamba Faid aliongoza uhalifu ambapo afisa wa polisi aliuawa, lakini akahukumiwa kwa uhalifu aliotekeleza mnamo Aprili.

Alikuwa amerudishwa jela 2011 kwa kukiuka masharti ya msamaha yanayohusiana na makosa ya awali.

Mwaka 2013, alitoroka katika jela ya kaskazini mwa Ufaransa ya Sequedin nje ya Lille, kwa kuwateka nyara walinzi wawili, lakini akakamatwa tena wiki sita baadaye

Mwaka uliopita, alihukumiwa kifungo cha miaka 10 jela kwa kutoroka jela 2013

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...