Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 02.07.2018


Juan Quintero

Wolves wamejaribu kumasaini kiungo wa kati wa Colombia Juan Quintero ambaye ameonyesha mchezo mzuri kwenye Kombe la Dunia nchini Urusi lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka Real Madrid na Tottenham kwa mchezaji huyo wa miaka 25. (Mirror)



Chelsea wanamteua meneja mpya Maurizio Sari leo Jumatatu na mchezaji ambaye atamsaini kwanza ni kiungo wa kati wa Urusi Aleksandr Golovin, 22, ambaye atagharimu pauni milioni 27 kutoka CSKA Moscow. (Sun)


Alassane Plea

West Ham na Fulham wanamenyana kwa pauni milioni 25 kumsaini mshambuliaji wa Nice Mfaransa Alassane Plea, 25. (Sun)



Newcasle pia nao wanammezea mate mshambuliaji wa zamani wa Lyon Plea, ambaye alifunga mabao 21 kwenye mashindano ya msimu uliopita. (Shields Gazette)


Andros Townsend

Newcasle wanatathmini ofa kwa wing'a wa Crystal Palace muingereza Andros Townsend, 26, lakini ikiwa tu wataamua kumuuza wing'a msikochi Matt Ritchie, 28, kwenda Stoke City. (Telegraph)


Juventus wamekataa ofa ya Lazio ya pauni milioni 89 na kiungo wa kati wa Uruguay Rodrigo Bentancur, 21 kwa kiungo wa kati wa Serbia Sergej Milinkovic-Savic, 23. (Tuttosport - in Italian)


Matej Vydra

Matej Vydra anakaribia kuhamia Leeds kwa pauni milioni 11 baada ya mshambuliaji huyo wa miaka 26 kutolewa kutoka kambi wa mazoezi ya Derby huko Tenerife. (Telegraph)

Stuttgart hawatamuuza mlinzi mfaransa Benjamin Pavard, 22, kwa milioni euro 50 na wanataka kumweka mchezaji huyo kwa mwaka mwingine kulingana na mkurugenzi wa klabu hiyo ya Ujerumani. (Stuttgarter Nachrichten - in German)

Liverpool imeanza tena mazungumzo na Lyon kwa ajili ya kiungo mshambuliaji Nabil Fekir, 24. (Sunday Mirror)


Nabil Fekir

Lakini Manchester United pia inamuhitaji mchezaji huyo.(La Progres - via Sunday Express)

Chelsea inatarajia kumtangaza meneja wa zamani wa Napoli Maurizio Sarri kuwa meneja wao mpya juma lijalo. (Talksport)



Tottenham wanampango wa kumnyakua kiungo mshamuliaji wa River Plate na timu ya taifa ya Colombia, Juan Quintero, 25. (La Nueva - via 90min)

Leicester City wamemteua Jacques Bonnevay kuwa meneja msaidizi wakati Michael Appleton akiondoka. (Leicester Mercury)


Michael Appleton

Mlinda mlango Thibaut Courtois yuko tayari kuondoka Chelsea ikiwa mbelgiji huyo atatimiza ndoto zake kuelekea Real Madrid. (Sunday Mirror)

The Blues wanasuka mipango ya kumnyakua mlina mlango wa Roma Alisson, 25 kwa kitita cha pauni milioni 65 wakiwa na mashaka ya kumpoteza Courtois. (Mail on Sunday)

Mlinda mlango wa Arsenal Petr Cech, 36, amesema Napoli imeonyesha kumuhitaji lakini yeye ana mpango wa kubaki Emirates. (Calcio Mercato)

Arsenal wanajiandaa kukamilisha mazungumzo kuhusu kumsajili kiungo mshambuliaji wa Uruguay Lucas Torreira, 22 kutoka Sampdoria juma lijalo. (Mail on Sunday)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...