Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wapalestina warudi kufanya ibada katika eneo takatifu

MTEULE THE BEST

Wanaoabudu walijaa katika eneo la jumba hilo baada ya viongozi wa Kiislamu kuondoa marufuku ya kususia ya wiki mbili kufuatia hatua hiyo ya Israel.
Wanaoabudu walijaa katika eneo la jumba hilo baada ya viongozi wa Kiislamu kuondoa marufuku ya kususia ya wiki mbili kufuatia hatua hiyo ya Israel.
Wapalestina wamerudi katika eneo muhimu la kufanya ibada mjini Jerusalem kwa mara ya kwanza katika kipindi cha wiki mbili baada ya Israel kuondoa vizuizi vya kiusalama.
Wanaoabudu walijaa katika eneo la jumba hilo baada ya viongozi wa Kiislamu kuondoa marufuku ya kususia ya wiki mbili kufuatia hatua hiyo ya Israel.
Mpango huo uliwekwa na Israel baada ya mauaji ya maafisa wawili wa polisi ya Israel karibu na eneo hilo.
Vizuizi vya mwisho viliondolewa siku ya Alhamisi baada ya siku kadhaa za ghasia ambapo watu saba waliuawa.
Wapalestina wamepinga kwa nguvu kuwekwa kwa vizuizi hivyo vya kiusalama ,wakidai kuwa ni jaribio la Israel kudhibiti mji huo wa zamani unaojulikana na Waislamu kama Harma al-Sharif huku Wayahudi wakiliita hekalu la mlimani.
Makundi ya raia wa Palestina walionekana wakiimba na kucheza densi katika eneo hilo kabla ya kuingia ndani kwa sala ya mchana.
Kulikuwa na ripoti za baadhi ya ghasia katika barabara nyembamba huku maafisa wa mipakani wakijaribu kudhibiti watu hao.
Vizuizi hivyo viliendelelea leo asubuhi, siku mbili baada ya mitambo ya kutambua vyuma kuondolewa.
Vizuizi hivyo viliendelelea leo asubuhi, siku mbili baada ya mitambo ya kutambua vyuma kuondolewa.
Vizuizi hivyo viliendelelea leo asubuhi, siku mbili baada ya mitambo ya kutambua vyuma kuondolewa.
Mzozo uliibuka baada ya polisi wawili wa Israel kuuawa karibu wiki mbili zilizopita.
Israel imesema kuwa itachukua hatua zisizokuwa na vizuizi miezi sita ijayo
Kumekuwa na makabiliano ya kila siku kati ya vikosi vya usalama vya Israel na waandamanaji tangu mitambo ya kutambua chuma iwekwe baada ya kuuwawa kwa polisi tare 14 mwezi huu karibu na eneo hilo la Haram al-Sharif kwa waislamu na Temple Mount kwa wayahudi.
Wapalestina wanne waliuawa na raia watatu wa Israel kuuliwa kwa kuchomwa visu na Mpalesina ambaye alidai alikuwa akilipiza hatua za Israel eneo katika eneo hilo takatifu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...