Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mjuwe Kansela Merkel Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameshinda tena katika uchaguzi wa Jumapili tarehe 24 Septemba, akirejea mara ya nne madarakani

MTEULE THE BEST

Mjuwe Kansela Merkel

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameshinda tena katika uchaguzi wa Jumapili tarehe 24 Septemba, akirejea mara ya nne madarakani. Lakini amewezaje kuufikia wadhifa huo muhimu wa kisiasa na sifa zake hasa ni zipi?
CDU-Wahlkampf mit Angela Merkel (picture-alliance/dpa/F. Gentsch)
Kansela Angela Merkel aliweka historia mara tu baada ya kuapishwa kuwa kansela mnamo mwezi Novemba mwaka 2005. hakuwa tu ni mwanamke wa kwanza kushikilia wadhfa huo wa Ukansela bali alikuwa ni kansela wa kwanza aliyetokea mashariki mwa Ujerumani eneo ambalo hadi mwaka 1990 lilikuwa linaongozwa kwa siasa za kisoshalisti.  
Tangu Merkel alipochukua madaraka, bila shaka ameweka alama ya sifa katika siasa za Ujerumani. Aliondoa hatua kwa hatua mpango wa nishati ya nyuklia, aliondoa sheria ya kuhudumu katika jeshi kwa lazima na alianzisha mafao kwa akina baba ambao hukaa nyumbani kwa muda mrefu ili kuwalea watoto wao, sera hizi zilimfanya apate uungwaji mkono kwa wingi hata kutoka kwenye vyama vya upinzani.
Deutschland Angela Merkel und Joachim Sauer (picture-alliance/dpa/T. Hase)
Kanselawa Ujerumani Angela Merkel na mumewe Joachim Sauer
Kansela Merkel pia ni kiongozi anayeheshimiwa katika bara Ulaya na kwingineko. Mnamo 2016, gaueti la Marekani la New York Times ililimtaja bi Merkel kuwa ni mmoja wa watetezi wa uhuru waliobakia ulimwenguni. Merkel aliongoza mjadala kati ya viongozi wa Ulaya wakati wa mgogoro wa sarafu ya Euro wa mwaka 2010.
Kansela Angela Merkel alipendekeza hatua kali kwa ajili ya kuziokoa nchi kama vile Ugiriki ili zisifilisike. Wakosoaji walisema hatua hizo zimesababisha umasikini na ukosefu wa ajira. Mwaka 2015, Bi Merkel aliwashangaza Wajerumani wengi na majirani zake katika nchi za Ulaya pale alipofungua mipaka ya Ujerumani kwa wahamiaji karibu 900,000 kutoka Syria, Afghanistan na mahali pengine.

Wakosoaji wa Bibi Merkel wanalalamika kwamba alishindwa kutekeleza mageuzi katika ya sekta ya afya na katika mfumo wa pensheni ili kuepuka hasira ya umma. Wanasema pia Merkel anabadili misimamo yake ya kisiasa kwa haraka ili aendelee kuwa maarufu. Kwa mfano, Bi Merkel wakati mmoja alikuwa anaunga mkono matumizi ya nishati ya atomiki. Baada ya ajali kwenye kinu cha nyuklia cha Fukushima huko Japan mnamo mwaka 2011 akageuka na kusema kuwa ni muhimu kukifunga.
Binz Wahlkampf CDU - Merkel (Reuters/A. Schmidt)
Mwanaume akiwa na bango linalosema kansela Angela Merkel aondoke.
Mpinzani wake mkuu katika uchaguzi wa mwaka huu Martin Schulz,amemlaumu mara kwa mara kwa kuepuka mijadala wa umma na kueleza wazi misimamo yake. 
Bi Merkel ameahidi kutumikia muda kamili wa miaka minne kama kansela iwapo chama chake kitashinda  katika uchaguzi wa Jumapili tarehe 24 mwezi Septemba mwaka huu wa 2017. Nafasi hiyo itaweza kumfanya kuwa kansela wa pili atayehudumu kwa kipindi kirefu tangu kumalizika Vita Kuu ya pili.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...