Msigwa aachiwa baada ya kukamatwa na Polisi Tanzania

MTEULE THE BEST
Peter MsigwaHaki miliki ya pichaTWITTER @MSIGWAPETER
Image captionMbunge wa Iringa Peter Msigwa
Polisi mjini Iringa imemuachia mbunge wa Iringa mjini Peter Msigwa kwa sharti la kumtaka arudi polisi Jumatatu.
Taarifa zinasema mbunge huyo ambae pia ni mchungaji wa kanisa alikamatwa pindi alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika eneo la Mlandege huko Mkoani Iringa.
Kwa mujibu wa msemaji wa Chadema Tumaini Makene, polisi inadai kumkatama Msigwa kwa tuhuma za uchochezi.
Msingwa anatoka chama cha Chadema ambacho ndio chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na kamata kamata ya wabunge nchini Tanzania kutoka upinzani hasa Chadema.
Miongoni mwa waliokumbwa na kamata hiyo hivi karibuni ni mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ambae hivi sasa yuko nchini Kenya kwa ajili ya matibabu baada ya kupigwa risasi na watu ambao mpaka sasa hawajafahamika huko Dodoma, bungeni.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU