Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Viongozi wa Ulaya wakutana kuzungumzia 'mfumo wa dijitali'

MTEULE THE BEST

Viongozi wa Ulaya wakutana kuzungumzia 'mfumo wa dijitali'

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanakutana mjini Tallinn, Estonia, kuzungumzia "mfumo wa dijitali" licha ya kugubikwa na mjadala uliotokana na mapendekezo ya rais wa Ufaransa kuhusu mustakbali wa Umoja huo.
Estland Tallinn EU-Gipfel Digital Summit 28.09.2017 (Reuters/V. Mayo)
Majadiliano yatakayoanza jioni ya leo (Septemba 29) yanatarajiwa kugubikwa na pendekezo la Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa la jinsi ya kutozwa ushuru makampuni makubwa makubwa ya kidijitali mfano wa Apple au Google, yanayotuhumiwa kutolipa ipasavyo kodi ya mapato.
Ufaransa inapendelea kuona makampuni makubwa makubwa mfano wa Google au Apple yakitozwa ushuru unaostahiki badala ya mtindo unaotumika hivi sasa wa kutozwa katika nchi moja tu ya Umoja wa Ulaya, mfano wa Ireland au Luxemburg, kodi ya mapato kwa shughuli za kibiashara walizofanya katika nchi zote za Umoja wa Ulaya.
Mada hiyo italeta malumbano katika mkutano huo wa kilele, ingawa haijaorodheshwa katika ajenda ya mazungumzo.
Lakini mbali na dijitali, suala la mustakbali wa Umoja wa Ulaya linategemewa kuhodhi mazungumzo mnamo wakati ambapo Umoja wa Ulaya unatafakari njia ya kufuata baada ya jinamizi la Brexit.
Kansela Angela Merkel na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron
Kansela Angela Merkel na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron
Umoja wa Ulaya unaokwenda kwa kasi tofauti
Mada hiiyo ililetwa mazungumzoni katika karamu ya chakula cha usiku jana ambapo viongozi wa Umoja wa Ulaya walizungumzia hotuba ya Macron aliyoitoa katika Chuo Kikuu cha Sorbonne mjini Paris Jumanne iliyopita, akiunga mkono fikra ya kuwepo kwa "Umoja wa ulaya wa kasi za aina tofauti" utakaoendelea kuwa chini ya usukani madhubuti wa Ufaransa na Ujerumani.
"Mimi ninaona kwamba katika hotuba yake hiyo, rais wa Ufaransa ameweka msingi imara wa kuendelezwa ushirikiano kati ya Ujerumani na Ufaransa," alisema Kansela Angela Merkel wa Ujerumani jana usiku na kuongeza ufafanuzi zaidi unahitajika na kwamba nchi hizo mbili zinakubaliana kuwa Umoja wa Ulaya unahitaji kufanyiwa marekebisho.
Viongozi hao wa Ujerumani na Ufaransa walizungumza ana kwa ana kwa muda wa nusu saa jana usiku, bila ya kuyajadili kwa kina mapendekezo ya rais wa Ufaransa, hasa kuhusu kanda ya Euro.
Mwishoni mwa karamu ya chakula cha usiku, viongozi wa Umoja wa Ulaya walielezea azma yao thabiti ya "kuuendeleza umoja" ndani ya Umoja wa Ulaya.
May anashiriki mkutano wa Tallinn
Mwenyekiti wa Baraza la Ulaya, Donald Tusk, atashauriana na viongozi wenzake wiki mbili kutoka sasa kuhusiana na mapendeko ya rais wa Ufaransa kuhusu sera ya pamoja ya uhamiaji.
Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May na mwenyekiti wa baraza la Ulaya Donald
Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May na mwenyekiti wa baraza la Ulaya Donald Tusk
Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May, pia alialikwa katika karamu hiyo ya chakula cha usiku.
Uingereza, inayojiandaa kuachana na Umoja wa Ulaya, haikuwa ikialikwa katika mikutano ya hivi karibuni inayozungumzia mustakbali wa Umoja huo.
Leo asubuhi, May alikutana na Rais Macron katika kituo cha Jumuiya ya Kujihami ya NATO mjini Tapa, walikowekwa wanajeshi wa Uingereza na Ufaransa.
Baadaye walitazamiwa kuelekea Tallinn kuhudhuria mkutano wa kilele kuhusu digitali

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...