MTEULE THE BEST Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionHugh Hefner alifariki kwa amani nyumbani kwake
Hugh Hefner, mwanzilishi wa jarida la kimataifa la watu wazima - Playboy, amefariki akiwa na umri wa miaka 91.
Playboy Enterprises Inc imesema alifariki kwa amani nyumbani .
Hefner alianza kuchapisha jarida hilo jikoni nyumbani mwake mnamo 1953. Likawa jarida linalo uzika zaidi la wanaume duniani.
Cooper Hefner, mwanawe amesema "atakumbukwa kwa ukubwa na wengi".
Alimtaja babake kama "Mojawapo ya watu wa kwanza kujitosa katika uandishi na aliishi maisha ya aina yake na yenye utofuati," na amemuita mtu anayetetea uhuru wa kuzungumza, haki za kiraia na uhuru wa kijinsia.
Mnamo 2012, akiwa na umri wa 86, alimuoa mke wake wa tatu Crystal Harris - ambaye alikuwa mdogo wake kwa miaka 60.
Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionMkewe wa wa tatu Crystal Harris anamrithi
Jarida la Hefner lilichangia kile kinachoonekana kuwa kuheshimiwa kwa picha za utupu katika vyombo vya habari na hilo lilimtajirisha na kumfanya kuwa milionea.
Ufanisi wake ukamuezesha kufungua maenoe ya kucheza kamari na vilabu vya burudani.
Tajiri huyo aliyeonekana mara nyingi akivaa nguo za hariri, aliishi maisha ya starehe, akiwachumbia na kuwaoa wanamitindo wanaopigwa picha katika jarida hilo .
Katika miaka yake ya baadaye alifurahikia kuandaa tamasha kubwa na mikusanyiko ya starehe katika majumba yake ya kifaharai.
Anadai kulala na zaidi ya wanawake 1000 na amesifia nguvu zake kwa dawa za kuongeza nguvu za kiume Viagra
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.
Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...
Maoni